UZINDUZI WA MBIO ZA MWENGE SONGEA MKOANI RUVUMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akiwasha Mwenge wa uhuru leo mjini Songea katika Uwanja wa Majimaji ikiwa ni sehemu ya sherehe za uzinduzi wa mbio za Mwenge kwa mwaka 2015
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akihotubia leo mjini Songea wakati wa sherehe za uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa uhuru zilizofanyika kitaifa mkoani Ruvuma.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein (kushoto)akimkabidhi  Kiongozi wa Wakimbiza Mwenge Kitaifa Juma Khatibu Chum (kulia)  Mwenge wa uhuru leo mjini Songea baada ya uzinduzi wa mbio hizo Kitaifa mkoani Ruvuma.
 Kiongozi wa Mbio za Mwenge kwa mwaka 2015 Juma Khatibu Chum(kushoto) akimkabidhi  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu(kulia)  Mwenge wa uhuru leo mjini Songea baada ya uzinduzi wa mbio hizo Kitaifa mkoani Ruvuma.
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu(kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Songea Profesa Norman Sigalla King(kulia) Mwenge wa Uhuru uhuru kwa ajili ya kuanza mbio wilayani humo baada ya uzinduzi ulifanywa leo mjini Songea  na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akihotubia leo mjini Songea.
Wananchi wa Mji wa Songea na Vijiji jirani na Mjihuo wakiwa katika uwanja wa Majimaji Mkoa wa Ruvuma kushuhudia uzinduzi wa mbio za  Mwenge wa Uhuru Kitaifa uliowashwa na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
Maafisa mbali mbali wakiwa katika uzinduzi wa Mbio za mwenge kitaifa uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein leo katika Uwanja wa  Majimaji Songea Mkoa wa Ruvuma

NAIBU WAZIRI WA MAJI MH AMOS MAKALLA AZINDUA MRADI MKUBWA WA MAJI KIJIJI CHA MKONGO NAKAWALE


Naibu Waziri wa Maji Mh. Amos Makalla akisalimiana na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo, kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Bi. Agnes Hokororo.


Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla amefanya ziara ya kikazi wilaya ya Namtumbo pamoja na mambo mengine amezindua mradi mkubwa Maji kijiji cha Mkongo Nakawale ambao watu zaidi ya 4000 wanapata Maji safi.

Aidha amekagua mradi wa Maji Milonji na ametoa agizo hadi kufikia tarehe 12 mei mwaka huu mkandarasi awe amekamilisha kuchimba kisima kingine baada kisima cha awali kuwa na Maji machache.


Pia Mh Makalla amemwagiza Katibu mkuu wizara ya Maji kuunda kikosi kazi cha watalaam kwenda Namtumbo kufuatilia matumizi ya Fedha kwa miradi ya Maji wilaya ya Namtumbo.
Naibu Waziri wa Maji Mh. Amos Makalla akisalimia watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo mara baada ya kuwasili Namtumbo kukagua na kuzindua miradi ya maji wilayani Namtumbo. Kushoto kwa Naibu Waziri ni Mkuu wa Wilaya Bi. Agnes Hokororo.
Naibu waziri wa Maji Mh. Amos Makalla akifungua maji katika moja ya vituo vya kuchotea maji bara baada ya uzinduzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Nakawale kilichopo Namtumbo mkoani Ruvuma.
Naibu Waziri wa Maji Mh. Amos Makalla akiwa na Mbunge wa Namtumbo Mh. Vitta Kawawa wakiashiria kuzinduliwa kwa mradi wa maji wa kijiji cha Nakawale.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

KAMPUNI ZISIZOSAJILIWA SOKO LA HISA KUBANWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
SERIKALI imesema katika siku zijazo haitoruhusu kampuni yoyote isiyosajiliwa katika Soko la Hisa kutolipa kodi na hata kutiliwa shaka kwamba shughuli zifanywazo haziko katika hali ya uwazi.
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alisema hayo Dar es Salaam na kuongeza kuwa ni vyema wamiliki wa kampuni mbalimbali nchini wakajiandaa kisaikolojia na kuhakikisha kampuni zao zinaandikishwa katika Soko la Hisa ili kuwezesha jamii kutambua kazi wazifanyazo kuwa ni za uwazi na zenye manufaa kwao.
“Kampuni mbalimbali…mtengeneze utaratibu wa kuingia katika Soko la Hisa Tanzania ili kuwezesha wananchi kiuchumi na pia kuondoa dhana kuwa mnaendesha shughuli zenu kwa usiri mkubwa,” alisema Nchemba.
Alisema Taifa linakokwenda si tu halitoruhusu kampuni kutolipa kodi bali hata kutiliwa shaka kwamba zinafanya shughuli zisizokuwa na uwazi. “Ni bora shughuli zenu mnazofanya ziweze kuungwa mkono na Watanzania wote.”
chanzo:Habari Leo
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa