LOWASSA AZIDI KUPATA MAPOKEZI MAKUBWA KILA ANAKOKWENDA, SONGEA ALAZIMIKA KUKAA JUU YA PAA LA NYUMBA‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAZIRI Mkuu Mstaafu,Edward Lowassa amesema hana shaka na swala la kukatwa jina lake katika vikao vya Chama cha Mapinduzi(CCM), kwani anaamini Chama chao kitatenda haki kwa kurudisha jina lake kuwa mgombea urais wa Tanzania.

Lowassa ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wa Mkoa wa Ruvuma katika ofisi kuu za CCM Mkoani humo, wakati akitoa shukrani baada ya kudhaminini na wanaCCM zaidi ya elfu 52.

"Nimekuwa mwanaCCM tangu mwaka 1977 nilipomaliza chuo kikuu, sijawahi kufanya kazi nje ya CCM hivyo nakijua chama na hakuna mgombea atakayeweza kuvunja rekodi ya utendaji wangu katika chama, sasa leo anayetaka kukata jina langu anatoka wapi? anakata kwa sababu gani? Sioni kosa la kukatwa jina na Watanzania hawaoni, kwa hiyo msiwe na wasiwasi jina litarudi tu". alisema Lowassa.

 Lowassa aliwasili Mkoani Ruvuma mapema mchana wa leo akitokea Mkoani Iringa kwaajili ya kusaka wadhamini katika mbio zake za kusaka urais kwa tiketi ya chama hicho, ambapo umati wa watu ulifurika kumlaki na kupelekea kufunga barabara kuu ya mjini, hali iliyompelekea Lowassa kupanda juu ya kibambaza cha jengo la ofisi ya CCM Mkoa ili aweze kuzungumza hao.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa, akizungumza na Umati wa WanaCCM pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma waliokuwa wamesimama nje ya Ofisi za CCM Mkoa huo, mjini Songea leo Juni 21, 2015, wakati alipofika kwa ajili ya kupata udhamini utakaomuwezesha kupata ridhaa ya Chama chake kuwania Urais kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akiwasalimia wanaCCM na Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma. 
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Chifu wa Kabila ya Wangoni, Chifu Ally Yussuf Songea (97). Chifu huyo alikwendwa kwenye uwanja wa Ndege wa Songea kumpokea Mh. Lowassa.
Wakinamama wa Mkoa wa Ruvuma wakimfurahia Mh. Lowassa.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akiwapungia mkono wanaCCM pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma.
Mmoja wa Wazee wa Mkoa wa Ruvuma, Mzee Ally Jaibu Rashid akitoa neno kwa niaba ya Wazee wa Ruvuma.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akizungumza machache na Wazee wa Mkoa wa Ruvuma.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akiondoka kwenye viwanja vya CCM Mkoa wa Ruvuma.

WAZIRI BERNARD MEMBE AENDELEA KUPATA UDHAMINI WA KISHINDO KATIKA MKOA WA RUVUMA‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (katikati) akilakiwa na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliofika kumpokea nje ya Ofisi ya CCM Mkoa wa Ruvuma iliyopo mjini Songea jana, baada ya kuwasili mkoani humo kwa ajili ya kutafuta wadhamini watakaotia saini fomu zake za kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, ambapo aliweza kupata wadhamini zaidi ya 5,000.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe akiwapungua mkono wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wananchi, waliofurika nje ya Ofisi ya CCM Mkoa wa Ruvuma iliyopo mjini Songea jana, baada ya kuwasili mkoani humo kwa ajili ya kutafuta wadhamini watakaotia saini fomu zake za kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, ambapo aliweza kupata wadhamini zaidi ya 5,000.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (kushoto) akilakiwa na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na vijana, waliofika kumpokea katika Uwanja wa Ndege wa mjini Songea jana, baada ya kuwasili mkoani Ruvuma kwa ajili ya kutafuta wadhamini watakaotia saini fomu zake za kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, ambapo aliweza kupata wadhamini zaidi ya 5,000. Picha zote na John Badi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (kushoto) akisoma moja ya mabango yenye ujumbe mbalimbali yaliyobebwa na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na vijana, waliofika kumpokea katika Uwanja wa Ndege wa mjini Songea jana, baada ya kuwasili mkoani Ruvuma kwa ajili ya kutafuta wadhamini watakaotia saini fomu zake za kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, ambapo aliweza kupata wadhamini zaidi ya 5,000.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma, Odo Mwisho akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe, fomu zilizotiwa saini na wanachama wa CCM mkoani humo, waliofika kwenye Ofisi hizo jana, kwa ajili ya kumdhamini ili ateuliwe kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, ambapo aliweza kupata wadhamini zaidi ya 5,000.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe, akizihakiki fomu zilizotiwa saini na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma, kwa ajili ya kumdhamini ili ateuliwe kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, baada ya kukabidhiwa na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo, Odo Mwisho (wa pili kulia), katika Ofisi za chama hicho mjini Songea jana, ambapo aliweza kupata wadhamini zaidi ya 5,000.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Ruvuma, waliofika kwenye Ofisi ya CCM zilizopo mjini Songea jana, kwa ajili ya kutia saini fomu za kumdhamini ili ateuliwe kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, ambapo aliweza kupata wadhamini zaidi ya 5,000.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (watatu kushoto), akipongezwa na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Ruvuma, waliofika kwenye Ofisi ya CCM zilizopo mjini Songea jana, kwa ajili ya kutia saini fomu za kumdhamini ili ateuliwe kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, ambapo aliweza kupata wadhamini zaidi ya 5,000. Wa pili (kushoto) ni Mkewe, Mama Dorcas Membe.
Wazee wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Ruvuma, wakimuembea dua maalum Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (kushoto), kwa ajili ya kumtakia kheri katika safari yake ya kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya kupata wadhamini kutoka mkoa huo jana. Wa pili (kushoto) ni Mkewe, Mama Dorcas Membe.
John Badi
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa