VIDEO:TAMASHA LA MAJIMAJI SEREBUKA KUTIMU VUMBI JULAI 22 HADI 30

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Msimu wa tatu wa tamasha la MAJIMAJI SEREBUKA linaloandaliwa na taasisi isiyo ya kiserikali Songea Mississipi, linatarajia kuanza julai 22 mwaka huu,Huku mishezo mbalimbali itahusishwa ikiwemo riadha,ngoma za asili,maonyesho ya kiabiahara na mdahalo,na nini hasa lengo la tamasha hilo huyu hapa mwenyekiti wa tamasha DAMASI NDUMBARO anabainisha. HABARI KAMILI HII HAPA VIDEO YAKE

VIDEO:FUKUTU LA UCHAGUZI WA VIONGOZI WA KLABU YA MAJIMAJI LA PAMBA MOTO.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Klabu ya MAJIMAJI inatarajia kufanya uchaguzi wa viongozi agust 5 mwaka huu ,ambao watakuwa na lengo la kuiongoza klabu hiyo na kuiletea maendeleo mkoa wa ruvuma kwa ujumla. Uchaguzi huo unafanyika baada ya viongozi wa awali kufikia kikomo wa kuiongoza klabu ya majimaji
https://youtu.be/xEZhepBTOnA HABARI KAMILI HII HAPA VIDEO YAKE

VIDEO:KAMTI HURU YA UCHAGUZI YA TIMU YA MAJIMAJI YA TANGAZA RATIBA YA KUCHUKUA FOMU.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Hatimaye kamati ya huru ya uchaguzi ya klabu ya MAJIMAJI imejitokeza mbele ya waandishi wa habari na kutangaza tarehe rasimi ya uchaguzi huo baada ya wanachama kushinikiza kufanyika kwa uchaguzi, ambapo nafasi zinazowania ni mwenyekiti wa klabu,makamu mwnyekiti wa klabu na mjumbe wa bodi HABARI KAMILI HII HAPA VIDEO YAKE.

VIDEO:MSIICHUKIE SERIKALI ILIYOPO MADARAKANI KWA KUKOSA AJIRA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Wanafunzi wa shirikisho la vyuo vikuu nchini wa chama cha mapinduzi wanaomaliza masomo yao wametakiwa kuacha kukichukia chama hicho kwa madai ya kukosa ajira kwani kufanya hivyo nikwenda kunyume na ilani ya chama.HABARI KAMIL HII HAPA VIDEO YAKE.

VIDEO:WAKAZI WA MJI WA SONGEA WAJITOKEZA KWA WINGI KUCHANGIA DAMU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kila ifikapo juni 14 ya kila mwaka ni siku ya kuchangia damu kwa hiari ,katika mkoa wa ruvuma Wakazi wa manispaa ya songea wamejitokeza kwa wingi kuchangia damu Lakini licha ya wananchi kujitokeza kwa wingi manispaa ya MANISPAA YA SONGEA yakabiliwa na uhaba wa damu katika hospitali ya RUFAA YA MKOA WA SONGEA,KITUO CHA AFYA MJIMWEMA kama anavobainisha msimamizi wa shughuli za mahabara MAGRETHI NGONYANI. HABARI KAMILI HII HAPA VIDEO YAKE.

JOKETI MWEGELO AKABIDHI MIFUKO 100 YA SARUJI KWA SHULE YA SEKONDARI YA MAPOSENI- RUVUMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

RTO RUVUMA ABEL SWAI “DEREVA BODABODA VAENI KOFIA NGUMU,ZINGATIENI SHERIA ZA BARABARABI”

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Ruvuma ABEL SWAI amewataka madereva pikipiki maarufu kama bodaboda kuvaa kofia ngumu katika kujinga na ajali za mara kwa mara wawapo barabarani kwa undani wa habari hii , Hii hapa video yake.

DC JUMA HOMERA AFANIKIWA KUANZA UJENZI WA KITUO CHA AFYA NAKAYAYA, TUNDURU.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
AOMBA WANANCHI PAMOJA NA WADAU MBALIMBALI WAMUUNGE MKONO KUFANIKISHA AZMA YAKE

Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Mhe. Juma Zuberi Homera ameazisha ujenzi wa kituo cha Afya Nakayaya, lengo la kuanzisha kituo hiki ni kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali ya wilaya Tunduru huzidiwa na wagonjwa kushindwa kupata matibabu kwa wakati.

Kata ya Nakayaya ipo umbali wa kilomita tano toka Tunduru mjini, kituo hiki kinatarajiwa kuhudumia kata ya Nakayaya, Masonya, Mlingoti na Nandembo/ Tarafa ya Mlingoti na Nampungu pamoja na maeneo ya jirani.

DC Homera alianzisha mchakato huo kwa kutafuta eneo la kujenga kituo na mara baada ya kupata eneo alimtafuta mchora ramani wa kituo cha afya na mara baada ya kupata ramani alitafuta vijana wa kusafisha eneo na hivi sasa mchanga wa kuanzia ujenzi upo eneo la ujenzi.

Jumla ya mifuko mia tatu ya saruji imepatikana, fedha bado zinakusanywa toka kwa wananchi, wafanyabiashara, makundi ya Vijana mbalimbali wa wilaya ya Tunduru,hivyo anawaomba wadau wengine wamuunge mkono.

Jumla ya matofali elfu thelathini zina hitajika ili kukamilisha ujenzi wa kituo hiki cha afya na zoezi la ufyetuaji utaanza hivi karibuni, vikundi mbalimbali vya vijana vinatarajia kuweka kambi ili kufanikisha zoezi hili.

Aidha, Dc Homera amewaomba wananchi wote waungane kufanikishe ujenzi wa kituo cha afya Nakayaya na hivi karibuni atatoa utaratibu wa kujitolea.

"Tunduru Mpya itajengwa na wenye moyo, wananchi wenzangu wa Tunduru nawaomba tuungane kujenga kituo hiki cha afya na hivi karibuni nitatoa utaratibu wa kujitolea kila mmoja Wetu, tumtangulize Mungu mbele tutafanikiwa kwa ushauri namna ya kufanikisha namba zangu ni +255759814088. Tumuuge mkono Rais wetu Mpendwa Dkt. John Pombe Magufuli katika kuwaletea maendeleo Watanzania nasi kwa upande Wa wana Tunduru tuna wajibika"
Mchoro wa kituo hicho kitakavyoonekana mara baada ya kukamilika.


Muonekano kwa nje itakavyokuwa.

Sehemu mbalimbali ndani ya kituo hicho kitakavyoonekana



VIDEO – WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MRUSHA ,HATARINI KUDONDOKEWA NA KUTA ZA MADARASA TUNDURU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Homera akimkabidhi mwanafunzi wa Shule ya msingi Mrusha Anna Nathan kwa niaba ya wanafunzi wenzake pesa kiasi cha shilingi elfu hamsini (50,000) kwa ajili ya kununua sukari ya kuweka katika uje wa wanafunzi. (Picha habari na Ruvuma TV ). Wanafunzi wa shule ya msingi Mrusha wilaya ya Tunduru mkoani Tuvuma wapo hatari kudondokewa na kuta za madarasa wanayoseomea kutona na madarasa hayo kuwa na nyufa za muda mrefu, Habari kamili hii hapa video yake.

VIDEO – ANAISHI KWA KULA MAFUTA YA KULA LITA MOJA, SUKARI ROBO TATU NA MAZIWA LITA MBILI KWA SIKU.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399..
SHUKURU KISONGA ni mtoto wa 5 kuzaliwa katika familia ya marehemu KISONGA yenye watoto 5, ni wanafunzi wa kidato chapili shule ya Sekondari MGOMBA iliyopo wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma.
Amezaliwa mwaka 2001 , akiwa na mwaka mmoja tangu azaliwe shukuru anakubwa na ugonjwa ambao hadi sasa haujafahamika ni aina gani ya ugonjwa unaomsumbua , Tangu akubwe na ugonjwa huo mwaka 2002 hadi leo hii amekuwa akila vyakula ambavyo vinawashangaza watu.
Kwa undani wa habari hii bonyeza play. Na kwa yule atakayeguswa na tatizo hili la motto huyu anaweza kuwasiliana na mama yake mazazi kwa namba ya simu 0742 322 408 ili aweze kupata matibabu.

VIDEO – KITUO CHA UTALII MKOA WA RUVUMA KUANDAA TAMASHA LA KUMTAFUTA MISS UTALII (BALOZI WA UTALII RUVUMA).

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Kituo cha utalii mkoa wa Ruvuma kinatarajia kuandaa tamasha la miss utalii mkoa wa Ruvuma, kwa kuwatumia wazawa kutoka wilaya za SONGEA,MBINGA,NYASA , TUNDURU na NAMTUMBO kwa lengo la kumpata balozi mmoja atakaye wakilisha kutangaza utalii uliopo katika mkoa wa huo.Hii hapa video yake.

SIMBA YA POKELEWA KAMA MFALME USIKU KATIKA WILAYA YA TUNDURU MKOANI RUVUMA, IKIELEKEA SONGEA MKOANI HUMO KUCHEZA NA MAJI MAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mashabiki wa Timu ya SIMBA SC wa Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma wakiwa wamejitokeza kwa wingi kuipokea timu yao ikitokea Dar , Mashabiki wa Simba hawakujali kuwa ni usiku walichokiona wao ni kuipokea timu yao kwa furaha , shangwe huku wengine wakiimba aungurumapo simba hucheza nani .....? pamoja na kuiombea ushindi wa nguvu.

Simba inakuja kucheza na Maji Maji ( Wanalizombe) tarehe 04 katika uwanja wa MAJI MAJI uliopo mjini Songea mkoani Ruvuma.

Utakuwa mchezo mkali na wa hatari sana maana simba inahitaji ushindi iweze kurudi juu na kushika msukani huku Maji Maji wakipambana kuhakikisha wanapanda juu zaidi ili waweze kunusurika na kushuka daraja ,

Umati wa mashabiki wa Simba katika Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma.

Tumekusogezea na VIDEO ya mapokezi ya Simba usiku huo huo katika wilaya ya Tunduru .HABARI KWA HISANI YA www.ruvumatv.com

VIDEO - WAJASIRIAMALI WASHAULIWA KUUNDA VIKUNDI WAWEZE KUJIUNGA NA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA (NHIF) ILI KURAHISISHA UPATIKANAJI WA MATIBABU PINDI WANAPOENDA HOSPITAL.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Wajasiriamali toka vikundi mbalimbali mkoani Ruvuma wamehamasishwa kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ili kurahisisha matibabu wawapo katika shughuli zao za kawaida, Wajasiriamali watakaojiunga na mfuko huo na kuwa wanachama watalipia shilingi 76,800 kwa mwaka ili kupata matibabu kupitia mfuko huo.

DC HOMERA AKAGUA MICHE ZA KOROSHO KWA AJILI YA MSIMU UJAO 2016/17

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Mhe. Juma Zuberi Homera,akiwa na baadhi ya wakulima wa Korosho
 Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Mhe. Juma Zuberi Homera,akishiriki kumwagilia miche ya zao la Korosho kwenye vitalu


Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Mhe. Juma Zuberi Homera, jana desemba  27,2016 alikwenda CDC kujiridhisha na uandaaji wa miche za mikorosho kwa msimu mpya wa Kilimo 2016/2017 na hatimaye kuridhishwa na maandalizi ya miche ya mikorosho iko ya kutosha na itaanza kusambazwa Kwa mujibu wa utaratibu wa uendelezaji wa zao hilo.

Lakini pia ametoa maelekezo kwa maafisa elimu. alisema, "maafisa elimu wanapaswa kuhakikisha wana kwenda sambamba katika uzalishaji wa zao hili la biashara wilayani Tunduru kwa upande wa shule za msingi na sekondari kwa kuandaa hekari 5 za mikorosho kila shule maafisa kilimo, watendaji wa Kata na vijiji wanapaswa kusimamia zoezi hili na mbegu hizo watagawiwa bure kama mradi wa EK na kuhusu uzalishaji wa mbegu mwaka huu ni mzuri zaidi ukilinganisha na mwaka jana. 
 
Mfano, kitalu cha CDC kina miche zaidi ya 79,000, kangomba zaidi ya miche 49,000, Mbesa zaidi ya miche 25,000, Nalasi zaidi ya miche 20,000, Namasakata zaidi ya miche 20,000, Misechela zaid ya miche 25,000, Muhuwesi 15000, Majimaji zaidi ya miche 10,000, Namiungo zaidi ya miche 15,000, Nandembo zaidi ya miche 15000, na kitanda zaidi ya miche15000 kazi kwetu wanatunduru mbegu hizi za kisasa zinazaa baada ya miaka 3".

Alisisitiza, "lakini pia ni mbegu bora kuhusu minada mpaka sasa wanunuzi mnada wa 4,5,6, wameshalipa bado kuwafikishia vyama vya msingi baada ya kufanya ukokotozi "TWENDE NA MKOROSHO WANGU UCHUMI WANGU" tusisahau kupanda mazao ya Chakula kama mahindi, mpunga, mihogo nk. Tumuunge mkono Rais wetu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika kuinua kilimo nchini na chenye tija kwa wananchi wanyonge na wa hali ya chini. HAPA KAZI TU mungu ni Mwema"

MHE. POSSI: JAMII IWASHIRIKISHE WATU WENYE ULEMAVU KATIKA FURSA ZOTE ZA MAENDELEO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na.Mwandishi Wetu
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu, Mhe. Dkt. Abdallah Possi ameiasa jamii kuwashirikisha watu wenye ulemavu katika shughuli zote za maendeleo ili kusaidia kuwainua na kuondokana na dhana ya utegemezi na kuwakwamua kiuchumi.
Dkt.Possi ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika Wilaya za Mbinga, Songea Vijijini na Nyasa mkoani Ruvuma ambapo alitembelea Shule zenye kuhudumia watu wenye mahitaji maalum za Songea Boys, Luhira, Huruma na Kituo cha Kulelea wenye ulewavu cha Peramiho Disabled Persons Action (PEDIPA) na Kituo cha kulele wazee na wenye ukoma cha Nge Wilayani Nyasa.
Katika ziara hiyo Mhe.Possi alibaini changamoto nyingi za watu wenye ulemavu na kuishauri jamii namna pekee ya kutatua changamoto wanazokabiliana nazo ni jamii kuona umuhimu wa kuwashirikisha watu hao katika mipango yote ya maendeleo.

“Halmashauri ziandae mipango ya kuwawezesha watu wenye ulemavu kuweza kushiriki kikamilifu katika kujitafutia kipato na hii itasaidia kuondokana na hali ya utegemezi na kuondoa mitazamo hasi juu ya watu wenye ulemavu kuwa hawawezi” .Alisema Mhe.Possi.

Waziri Possi alisisitiza kuwa ni lazima Halmashauri ziwe na ubunifu wa miradi ya maendeleo itakayo walenga watu wenye ulemavu, “Ni vyema sasa kuwe na jitihada za makusudi za kuunda miradi maalum kwa ajili ya kuwapa nafasi za ushiriki ili kujitafutia vipato na kuyakabili mazingira yao, ikumbukwe wakina mama waliachwa nyuma kwa muda mrefu ila baada ya kupaza sauti zao tunaona sasa wanasikika hivyo hivyo iwe kwa watu wenye ulemavu” Alisitiza Dkt.Possi.
Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nyasa Dkt.Osca Albano alisisitiza kuyapokea maelekezo yote ya Naibu Waziri Mhe.Possi kwa vitendo na kumhakikishia kuwa Wilaya yao itakuwa mstari wa mbele katika kulitekeleza hilo.
 “Sisi tunafanya kazi kwa ushirikiano mzuri na Halmashauri hivyo ni vyema tukalichukua hilo kuangalia namna tunavyoweza kuliweka katika mipango yetu yote ya maendeleo ili kuwasaidia na kufikia lengo la serikali,” alisema Dkt. Albano.
Nae Katibu Tawala Wilaya ya Songea Bw. Edmund Siame aliomba halmashauri zote ziwe zinatoa mrejesho mapema juu ya maagizo yanayotolewa na viongozi wa juu huku Mwalimu Elswida Charles anayehudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum akimweleza Dkt. Possi kuwa watu wenye ulemavu wanafarijika kutokana na jitihada anazofanya kuwainua watu wenye ulemavu.

VIDEO - NAIBU WAZIRI POSSI AWAPA UKWELI WAHITIMU AJUCO SONGEA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi.

VIDEO - WAKAZI WA MWENGE MSHINDO WA MUOMBA RAIS AWASAIDIE WAWEZE KULIPWA STAHIKI ZAO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Baadhi ya wananchi wa kata ya MWENGEMSHINDO Manispaa ya SONGEA mkoani RUVUMA ambao maeneo yao yamechukuliwa na MAMLAKA ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji nchini (EPZA) kwa kipindi cha miaka tisa iliyopita bila kuwalipa fidia yoyote, wamemuomba rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania DOKTA JOHN POMBE MAGUFULI kuingilia kati suala hilo ili waweze kupata haki yao.story kamili bonyeza hiyo video.

VIDEO- WAKULIMA WA ZAO LA KORSHO TUNDURU WANUFAIKA NA BEI MPYA YA ZAO HILO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh7m671y6bLV1959JfjkFmMXlz2n_74O1PXN1RZNGPetI9APnbo7kPPcQlteWIZe54vQy1sCiOaKXrM1P7BOWgrrX7QbDQ2T5p-2hv4r88s_MJut8o8CvTcVr3A3io2As6JNBUX6PpypD32/s1600/IMG_4156.jpg
WAKULIMA wa korosho Wilaya ya Tunduru, wameondokana na umasikini kutokana na kupata soko la uhakika baada ya Kampuni ya Namela General Trade kushinda zabuni ya kununua zao hilo wakulima kwa bei ya Sh 3,757 kwa kilo, ikizishinda kampuni nyingine saba.

Hadi kufikia Novemba 14, kulikuwa na zaidi ya tani 541 zilizoingizwa katika ghala la Chama Kikuu cha Ushirika Wilaya ya Tunduru (Tancu) ambako kampuni hiyo ilipewa kununua korosho tani 400 huku Kampuni ya Machinga iliyoshinda nafasi ya pili katika mnada huo, ikipata kibali cha kununua tani 141 kwa bei ya Sh 3,750.

Bei ya kununua mahindi yaongezwa

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
SERIKALI kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), Kanda ya Songea, imelazimika kuongeza bei ya kununulia mahindi ya wakulima mkoani Ruvuma kutokana na ushindani mkubwa, baada ya kuwepo kwa wanunuzi binafsi wengi wanaonunua mahindi kwa bei kubwa.
Kutokana na ushindani uliopo, NFRA kuanzia Novemba 7, mwaka huu ililazimika kupandisha bei ya kununua mahindi hadi kufikia Sh 580 kwa maeneo ya vijijini na Sh 600 kwa watakaoleta katika kituo kikuu cha Ruhuwiko mjini Songea.
Hayo yalisemwa na Kaimu Meneja wa NFRA Kanda ya Songea, Majuto Chabruma, alipozungumzia kazi ya ununuzi wa mahindi katika vituo mbalimbali vilivyotengwa katika wilaya zote za mkoa wa Ruvuma.
Chabruma alisema mwaka huu Serikali ilituma Sh bilioni 6.4 kwa ajili ya kununua mahindi tani 12,000 za awali huku malengo ikiwa ni kununua tani 22,000 na bado wanaendelea na kazi hiyo japo hawajafikia lengo lao.
Hata hivyo, kuna ushindani mkubwa wa soko kutoka kwa watu na kampuni binafsi ambazo zimeingia mkoani Ruvuma kwa ajili ya kununua mahindi.
Chabruma alisema serikali imeona ni vyema kuongeza bei ya mahindi ili kukabiliana na ushindani wa bei iliyopo sokoni, jambo lililosababisha kupungua kwa mahindi.
Alisema bado wakala unaendelea kununua ziada ya mahindi ambayo bado ipo kwa wakulima na wauzaji wengine katika kituo cha Ruhuwiko Songea na amewashauri wakulima mkoani Ruvuma ambao bado wana mahindi nyumbani kuyauza kwa wakala huo.
Alisema hatua hiyo itaiwezesha serikali kufikia malengo yake na nchi kwa jumla iwe na akiba na kuwezesha kutoa nafaka hiyo pindi kutakapojitokeza uhaba wa chakula nchini.
Aidha, Chabruma aliwakumbusha wakulima mkoani Ruvuma kuanza maandalizi ya msimu mpya wa kilimo wakati huu kwani mvua za kwanza zimeshaanza kunyesha katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo, pamoja na baadhi ya mikoa mingine nchini.

SERIKALI YATENGA BILIONI 13 KUWEKA MAJI SAFI RUVUMA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge  akijibu swali Bungeni leo mjini Dodoma.
Na Jacquiline Mrisho, Dodoma.

Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 13.17 katika Bajeti ya mwaka 2016/2017 kwa lengo la kutekeleza miradi ya maji katika vijiji vya mkoa wa Ruvuma ili kuhakikisha wananchi wa maeneo hayo wanapata maji safi na salama.

Kiasi hicho cha fedha kimetajwa leo mjini Dodoma na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge alipokuwa akijibu swali la Mhe. Jacqueline Ngonyani (Viti Maalum) lililohoji juu ya muda ambao Serikali itapeleka majisafi na salama katika Mkoa huo.


Waziri amesema kuwa Mpango wa Utekelezaji wa Maji Vijijini ulioanza mwaka 2006/ 2007, mkoa wa Ruvuma ulipangiwa vijiji 80 na kati ya vijiji hivyo jumla ya vijiji 76 vilipata maji safi na salama.  


“Asilimia kubwa ya vijiji vilivyokuwa katika miradi hiyo vimepata maji safi na miradi iliyobakia ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji hivyo kwa mwaka huu wa fedha Ruvuma imetengewa kiasi cha fedha cha bilioni 13.17 ili changamoto ya maji safi na salama katika mkoa huo iishe kabisa”, alisema Lwenge.


Ameongeza kuwa Serikali imeendelea na mipango ya kuboresha huduma hizo katika miji ya Songea, Mbinga, Namtumbo na Tunduru iliyopo katika mkoa huo ambapo kwa mji wa Songea, mradi wa ukarabati wa chanzo cha maji cha mto Ruhila Darajani umekamilika kwa gharama ya shilingi bilioni 2.6.


Amefafanua kuwa kukamilika kwa chanzo hicho mnamo mwezi Februari mwaka huu kumeongeza kiasi cha upatikanaji wa maji wa jumla ya lita milioni 6 kwa siku ambapo wakazi 164,162 wamenufaika katika Manispaa hiyo.


Aidha, Mhandisi Lwenge amebainisha kuwa kwa sasa Serikali imekamilisha usanifu wa kina na uandaaji wa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya uboreshaji wa huduma hizo katika miji iliyopo katika mkoa huo.


“Serikali inaendelea na jitihada ya kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo ambayo kwa mji wa Tunduru mradi utagharimu  Dola za Kimarekani milioni 7.3, mji wa Namtumbo ni Dola za Kimarekani 12.08, na Dola za Kimarekani 11.86 kwa ajili ya mji wa Mbinga”, alisema Mhandisi Lwenge.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa