MAHENGE AAGIZA KILA KATA KUJENGA ZAHANATI MOJA YA KIJIJI


Na Godfriend Mbuya
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dr. Binilith Mahenge amesema ameagiza kila kata kujenga zahati moja kwenye kijiji kimoja kila mwaka ili kurahisishia wananchi kupat huduma za afya na kuepuka adhan ya kutembea umbali mrefu tutafuta huduma.

Akizungumza na East Afrika Radio katika  kipindi cha SUPAMIX  Mahenge amesema kama kata ina vijiji vinne basi ndani ya miaka minne itakuwa na zahati kila kijiji, huku akisisitiza kuwa serikali ya mkoa imejipanga vizuri kuhakikisha inatatua matatizo makubwa matatu  suala la elimu, maji na afya.

“Wananchi wanatumia muda mwingi kwenda kwenye maji, wanachukua muda mwingi kwenda kwenye vituo vya afya pia muda mwingi watoto kwenda shuleni hivyo muda mwingi wa kufanya kazi kama ilivyo adhma ya serikali ya ‘Hapa Kazi Tu’ unatumika katika kupata huduma za kijamii jambo ambalo tunataka kuondokana nalo kwa kuelekeza nguvu zetu katika maeneo hayo”- Amesema Mahenge.
Aidha kuhusu namna serikali ya mkoa wake inavyosaidi vijana na wanawake Mkuu huyo wa Mkoa amesema agizo la serikali katika Halmashauri zote nchini kutenga asilimia 5% kwa wanawake na 5% kwa vijana linafanyiwa kazi hivyo makundi hayo yajiunge katika vikundi ili kuweza kupata fedha hizo.

DC TUNDURU JUMA HOMERA AWATIA MBARONI VIONGOZI 4 KWA TUHUMA ZA KUUZA VIWANJA.


Askari akiwa amewakamata Viongozi wawili wa Serikali ya Kijiji waliokuwa wakituhumiwa kwa ubadhirifu wa viwanja.

Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili Ndugu Japhet Muogopeni Mnyagala akizungumza mbele ya Wananchi .


Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Juma Zuberi Homera akizungumza na Wananchi wa Vitongoji vya FrankWeston na Umoja vilivyokumbwa na mgogoro wa ardhi.
Mkuu wa Wilaya Tunduru Mhe. Juma Zuberi Homera akimuagiza Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili Ndugu Japhet Muogopeni Mnyagala kuchukua hatua stahiki kuhusiana na mgogoro wa Ardhi ndani ya Wilaya hiyo.


Wananchi wakimsikiza kwa makini Mhe DC. Juma Zuberi Homera .
 
Mkuu wa Wilaya Tunduru Mhe. Juma Zuberi Homera, amewatia mbaroni Viongozi wanne wa Serikali ya vijiji kwa kosa la usimamizi mbovu wa ardhi katika Vitongoji vya Umoja na Frank Weston katika kata ya Nanjoka Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma.

Akisoma taarifa mbele ya Mkuu wa Wilaya Bw. Yahaya Issa Abdallah alimueleza DC. Homera kuwa Vitongoji vya Umoja na Frank Weston vimekumbwa na mgogoro wa ardhi kati ya Wenyeji, Wageni na Wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya Tunduru kwa muda mrefu.

Aidha Serikali kupitia Idara ya Ardhi na Maliasili Wilaya, iliwapimia ardhi Wananchi toka 11/08/2014 lakini ikabainika kuwa mpaka  30/06/2016 bado Wananchi hawakupewa maeneo yao na kuna baadhi ya Wafanyakazi wa Halmashauri pamoja na Wageni wapo kwenye orodha ya Wananchi wanaopaswa kugawiwa Viwanja.

Akihutubia kwenye mkutano huo wa hadhara, uliyofanyika katika Shule ya Msingi Umoja, DC Homera aliwaeleza Wananchi kuwa wasiwe na shaka,kwa sababu Serikali ipo upande wao na hakuna atakaye dhurumiwa haki yake, alisema “Namtaka Mhasibu wa Ardhi na Maliasili alete orodha ya waliolipia Ardhi maeneo ambayo siyo ya wakazi, na ambao ni Watumishi wa Halmashauri wafutwe kwenye orodha hiyo na warejeshewe fedha zao”.

Mfano, kuna baadhi ya watumishi wa Idara ya Ardhi na Maliasili,ambao wamefanya ujanja ujanja kinyume cha sheria kwa kuwaweka watoto wao kwenye orodha,na majina yao yameorodheshwa hapa,hivyo hatua za kisheria na taratibu zitafanyika kuondoa huu mgongano ambao umejitokeza katika hili pia. 
 Kama vile haitoshi ikabainika kuwa kuna kuna baadhi ya Viongozi walikusanya fedha  za wananchi  wapatao 522 na kutowapa risiti,jambo amablo ni hujuma za wazi kabisa  za kuikosesha Halmashauri ya Tunduru Mapato na kupelekea fedha kuwa mikononi mwa wajanja wachache.

Aidha aliwataka Wafanyakazi wa Idara ya Ardhi na Maliasili kujieleza ni kwa nini wamewagawia watu ardhi ambao sio wakazi? kwa nini wamefanya udanganyifu wa kuwa milikisha ardhi Watumishi wa Halmashauri kwa njia za rushwa? na kwa nini wananchi zaidi ya 522 hawajapewa maeneo yao kwa zaidi ya Miaka Miwili?

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili wa Wilaya ndg. Japhet Muogopeni Mnyagala alikiri kufanya kosa,lakini pia alimuakikishia Mkuu wa Wilaya ndani ya wiki moja wananchi wataanza kugawiwa viwanja na zoezi hilo litaanza Kesho (leo).

Mkuu wa wilaya aliwaagiza askari wakamate viongozi walio kuwa wasimamizi wa upimaji wa maeneo katika vitongoji vya Umoja na Frank Weston ambao ni Mohammed Dumsala, Matola Limelime, Halid Daud na Tekla Damas.

JKT Mlale yakabidhi madawati

JESHI la Kujenga Taifa (JKT), Kikosi cha 842 KJ Mlale kilichopo wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, kimekabidhi madawati 1,074 kukabiliana na upungufu katika jimbo la Peramiho na Madaba.
Madawati 534 yalikabidhiwa kwa Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama na mengine 540 yalikabidhiwa kwa Mbunge wa Madaba, Joseph Mhagama kwa ajili ya halmashauri ya wilaya ya Madaba na yatasambazwa katika shule zenye upungufu wa madawati.
Akikabidhi madawati hayo jana, Mkuu wa Kikosi cha 842 Kj, Meja Absolomon Shaushi alisema madawati hayo ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kuzitaka taasisi za serikali, mashirika na watu binafsi kusaidiana na serikali kupunguza uhaba uliopo ili watoto wasome vizuri.
Shaushi alisema kikosi kilipewa kazi ya kutengeneza madawati kwa ajili ya kukabiliana na upungufu uliopo kwa shule za msingi na hadi sasa kazi hiyo inaendelea vizuri kutokana na morali ya hali ya juu waliyonayo vijana hasa ikizingatiwa kuwa ni miongoni mwa waathirika wa uhaba wa madawati kwenye shule walizosoma.
Alisema kikosi kimejipanga vyema kuhakikisha kazi hiyo inafanyika kwa kuzingatia ubora unaotakiwa na kuziomba taasisi nyingine ambazo ziko tayari kumuunga mkono Rais Magufuli katika suala hilo kukitumia Kikosi cha Mlale JKT ambacho kina uwezo mkubwa katika utengenezaji wa madawati na samani nyingine kama vile milango, meza kwa ajili ya ofisi, vitanda na makabati.
Chanzo Na Habari Leo

Tutangaze vivutio vya kiutamaduni: Prof. Elisante Ole Gabriel

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

eli1 
Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma  Bw  Hassan Bendeyeko  akifungua kikao  kati ya wadau wa Sekta za Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo na Wizara husika kilichofanyika Mjini Songea Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel na  kulia ni Afisa Elimu MkoaBw.Gharama Kinderu
eli2 
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo akisikiliza maelezo ya baadhi ya vifaa vilivyotumika katika vita ya Majimaji kutoka kwa Afisa Elimu Makumbusho ya Taifa  Bi. Blantina Raphael wakati alipotembelea makumbusho hayo mjini Songea, katikati ni Afisa Elimu wa Mkoa wa Ruvuma  Bw.Gharama Kinderu. picha na Zawadi Msalla- WHUSM Ruvuma

Na Zawadi Msalla- WHUSM Ruvuma
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel ametoa wito kwa viongozi na wadau wa sekta ya Utamaduni wa Mkoa wa Ruvuma kutangaza Utamaduni na Utalii unaopatikana katika mkoa huo.
Wito huo umetolewa jana mjini Songea na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel alipokuwa akizungumza na wadau wa sekta za Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo katika ofisi za mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.
“Mkoa wenu una vivutio vingi vya asili vinavyoonesha tamaduni za wanaruvuma  ambavyo vikitumika vizuri ni fursa nzuri ya mapato” alisema Prof Gabriel.
Ameongeza kuwa Mkoa wa Ruvuma una vivutio vingi vya Utamaduni  vya kuvutia watalii ambavyo ni fursa nzuri ya kutangaza Utamaduni wa Mkoa na Tanzania kwa ujumla.
Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Bw.Hassan Bendeyeko alikiri kuwepo kwa changamoto ya kuvitangaza vivutio hivyo kutokana na ubovu wa miundombinu iliyopo .
Hata hivyo  alisema kuwa ujenzi wa miundombinu utasaidia vivutio hivyo kufikika kwa urahisi na wanategemea Mkoa huo kuinuka kiuchumi hasa baada ya changamoto hiyo kutatuliwa.
Bw.Bendeyeko alisema kuwa baadhi ya vivutio vya kiutamaduni vinavyo hitaji kutangazwa ili vifahamike ndani na nje ya nchi ni pamoja na Makumbusho ya Majimaji, eneo waliponyongwa wapiganaji wa vita vya majimaji, Ziwa Nyasa pamoja na mbuga mbali mbali.
Aidha alieleza kuwa wanatarajia kuajiri Maafisa Utamaduni wakutosha  katika kila Halmashauri ambapo  kwa kushirikiana na Maafisa Habari na waandishi wa habari kutangaza vivutio hivyo.

MBINGA WATAKIWA KUCHANGAMKIA NHIF

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) amewataka wajasiriamali mkoani Ruvuma kuchangamkia mpango maalumu wa matibabu wa Kikoa waweze kuhudumiwa kwa gharama ya Sh 90,000 kwa mwaka.
Ofisa Mwandamizi wa mfuko huo mkoani Ruvuma, Calytus Mpangala aliwaambia wajasiriamali kutumia fursa hiyo adimu iliyotolewa na serikali kupitia NHIF wawe na uhakika wa kupata huduma bora za matibabu bila kutumia fedha ya mfukoni.
Mpangala alikuwa akizungumza na wateja wa Benki ya Wananchi Mbinga (MCB) katika Wilaya ya Nyasa waliojiunga katika vikundi vya ujasiriamali.
Alisema NHIF inahamasisha wananchi waliopo katika vikundi maalumu vya kiuchumi kama vile vikundi vya kilimo, mama lishe, migahawa na vinginevyo kuchangia Sh 96,000 ambayo Sh 78,600 inakwenda bima ya afya.
Zilizobaki ni kwa ajili ya shughuli za uendeshaji, riba na gharama za wafuatiliaji ambao ni MCB ambao ni mawakala wa NHIF.
Mpangala alisema, kiasi hicho cha fedha kitamwezesha mwana kikundi kupata matibabu kuanzia kwenye zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya na mkoa na hata hospitali ya rufaa popote nchini pale mwanachama wa mfuko huo atakapohitaji kutibiwa, isipokuwa baadhi ya gharama kama usafiri, malazi na chakula zitakuwa za mwanachama mwenyewe.
Chanzo Gazeti la Habari leo
 

Aflatoxin yahatarisha afya za walaji

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.




UELEWA mdogo kuhusu aina ya sumu inayozalishwa na kuvu waishio kwenye udongo au mimea na nafaka zilizooza, umesababisha vita dhidi yake nchini kutofanikiwa ipasavyo hivyo kuhatarisha afya za walaji.
Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Florens Turuka alisema sumu hiyo ijulikanayo kama aflatoxins, inasababisha usalama mdogo wa chakula na inahatarisha afya kwa walaji .
Akizungumza jijini Dar es Salaam kwenye mkutano uliozungumzia mapambano dhidi ya sumu hiyo , Turuka alisema sumu hiyo pia inaharibu biashara ya bidhaa za mazao hasa nafaka.
Pamoja na mambo mengine, wajumbe wa mkutano huo walijadili namna bora ya kuhusisha mapambano ya sumu hiyo kwenye miradi, programu na mipango mbalimbali.
Dk Turuka alisema, serikali itatoa kila aina ya ushirikiano kuhakikisha kuwa juhudi zote za mapambano dhidi ya aflatoxin zinafanikiwa. Kwa mujibu wa Turuka, aflatoxin ni tatizo kubwa kwenye mfumo wa chakula nchini hususan kwenye mahindi, karanga na maziwa.
“Vyakula hivi ni kati ya vinavyoliwa kwa wingi hapa nchini,” alisema.
Alisema bado juhudi kubwa zinatakiwa kufanywa kuondokana na tatizo hilo ambalo huweza kusababisha saratani ya ini. Utafiti wa hivi karibuni umeonesha kuwa maeneo ya ukanda wa Mashariki na Magharibi nchini ndiyo yaliyoathirika zaidi na sumu hiyo katika mfumo wa vyakula.
Alishukuru Kamisheni ya Umoja wa Afrika kwa juhudi zake za kudhibiti sumu hiyo.
Pia alishuruku timu ya wadau wanaopambana na sumu hiyo (Partnership for Aflatoxin Control in Africa -PACA) kwa kuratibu mkutano huo. Licha ya Tanzania ambaye ni mwenyeji, mkutano huo ulihudhuriwa na wajumbe kutoka Gambia, Malawi, Senegal na Uganda.


Chanzo Gazeti la Habari leo

RUSHWA YA NGONO HUCHANGIA KURUDISHA NYUMA KASI YA MAENDELEO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

RUSHWA YA NGONO HUCHANGIA KURUDISHA NYUMA KASI YA MAENDELEO

 Mratibu wa Asasi ya kuinua maendeleo ya Jamii na Kuhifadhi Mazingira (Ececo)Ndosho Hamisi akisisitiza jambo wakati akitoa mada juu ya madhara ya rushwa ya ngono iliyofanyika kijiji cha Duga wilayani Mkinga iliyokuwa na lengo la kuwapa uelewa jamii ya wasichana wa wafuigaji wa kimasaia iliyofanyika
 Baadhi ya wananchi wa Kata ya Duga Maforoni wakifuatilia mada mbalimbalio zilizokuwa zikiwasilishwa
 Katibu wa Asasi ya Kuinua Jamii na Kuhifadhi Mazingira (ECECO TANZANIA),Said Kamba akisisitiza jambo kwa washiriki wa semina hiyo
 Diwani wa Kata ya Duga Maforoni Ally Ally akizungumza katika semina hiyo

IMEELEZWA kuwa rushwa ya ngono imekuwa ni tishio hapa nchini hali inayochangia kurudisha nyuma kasi ya maendeleo kwani imekuwa ikipunguza demokrasia na utawala bora kwa watanzania jambo ambalo linapaswa kupigwa vita kwa vitendo.

Hayo yalisemwa juzi na Mratibu wa Asasi ya Kuinua Maendeleo ya Jamii na Kuhifadhi Mazingira (Ececo), Ndosho Hamisi wakati wa semina ya rushwa ya ngono iliyofanyika Kijiji cha Maforoni Kata ya Duga wilayani hapa na kufadhiliwa na Women Fund Tanzania  (WTF)iliyokuwa na lengo la kuwapa uelewa juu mambo hayo kwa wasichana na wanawake hasa wa jamii ya wafugaji wa kimasai.

Alisema kuwa tatizo hilo limekuwa likichukua kasi kwenye sekta nyingi na kusababisha kukandamiza haki za wanaostahili kuweza kupata fursa za kuweza kupata nafasi za kukuza uchumi wao na hivyo wengi wao kuishia katika hali duni.

  “Ukiangalia leo hii unaweza kutaka kitu Fulani mahali lakini kwa sababu hauna sifa ambazo zinapaswa kukipata basi yanaweza kutumika mazingira ambayo sio sahihi ili uweze kukipata kutokana na kumtimizia mahitaji yake mlengwa na hili limekuwa tatizo kubwa “Alisema.

 “Ni kosa kisheria mtu mwenye mamlaka kumpandisha cheo mfanyakazi wake kutokana na kuwepo kwa mazingira ya rushwa ya ngono kwa sababu inasababisha kupunguza ufanisi kazini na hivyo kushindwa kupiga hatua kubwa za kimaendeleo “Alisema.

Alisema jambo hilo limekuwa na madhara mengi kwa jamii ikiwemo kupata magonjwa makubwa ikiwemo ukimwi lakini pia uzalilishaji kitendo ambacho kinapelekea kushusha utendaji na kuchangia kurudisha nyuma maendeleo.

Awali akizungumza wakati akifungua semina hiyo, Diwani wa Kata ya Duga, Ally Mohamed aliipongeza asasi hiyo kwa kuona umuhimu kuwapatia mafunzo hayo ambayo yataweza kuwapa uelewa juu ya madhara ya rushwa ya ngono na kubadilika

“Unaweza kukuta wakati mwengine watoto wadogo wanazalilika kutokana na kutokujua madhara ya rushwa ya ngono hivyo semina hii itawafungua macho kuona namna ya kuweza kupiga vita vitendo hivyo “Alisema

‘Acheni shughuli za binadamu kwenye vyanzo vya maji’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga, Venance Mwamengo, amepiga marufuku shughuli zote za kibinadamu kufanyika kandokando ya vyanzo vya maji kupunguza tatizo la uhaba wa maji ambalo limekumba eneo kubwa la wilaya hiyo.
Aidha Mwamengo, amezuia pia shughuli za kibinadamu ikiwamo kilimo katika milima jirani ya chanzo na mradi wa maji katika kijiji cha Kigonsera ambapo baadhi ya watu wamesababisha mradi wa maji katika kijiji hicho uliotumia kiasi kikubwa cha fedha kushindwa kufanya kazi.
Mwamengo alipiga marufuku shughuli hizo hivi karibuni wakati akizungumza na wananchi wa kijiji hicho na kuziagiza mamlaka zinazohusika kuhakikisha zinalinda vyanzo vyote vya maji kijijini hapo.
Pia aliwaagiza watendaji wa vijiji na kata, kuwasaka na kuwafikisha mahakamani watu wote waliosababisha mradi huo kushindwa kufanya kazi iliyokusudiwa licha ya serikali kutumia fedha nyingi kutekeleza mradi huo kuwaondolea wananchi kero hiyo ya muda mrefu.
Aliwataka watendaji hao, kuwashirikisha askari mgambo kufanya msako kabambe ambao utafanikisha kuwapata wahusika na pia kufanya doria ya mara kwa mara katika maeneo hayo muhimu kuzuia watu wachache wanaoharibu vyanzo hivyo.
“Kama watendaji mtashindwa kupata waharibifu hao wa vyanzo vya maji mimi mwenyewe kuanzia wiki ijayo nitaanza msako kuwatafuta watu ambao ni kikwazo katika mipango mingi ya maendeleo wilayani kwetu,” alisema Mwamengo.

Chanzo Gazeti la Habari Leo
 

Mbinga waukataa Mfuko wa Vidung’ata

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


HALMASHAURI ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma imeombwa kuufuta Mfuko wa Vidung’ata, unaohudumia wakulima wa kahawa wilayani humo.
Ombi hilo lilitolewa na wanachama wa Chama cha Ushirika wilayani Mbinga (MBIFACU).
Walisema hayo juzi katika mkutano wao kwa nyakati tofauti. Walisema mfuko huo umekuwa ukiwanufaisha baadhi ya watendaji waliopo serikalini na sio wakulima hao.
Kwamba makato ya fedha wanazokatwa katika kila msimu wa mavuno ya kahawa ni makubwa mno. Fedha hizo zililenga kununua dawa ya kuhudumia zao hilo, lakini cha kushangaza dawa hizo kwa ajili ya wakulima, zimekuwa haziwafikii. Lengo la kuunda Mfuko wa Vidung’ata ni kudhibiti wadudu wanaoshambulia mti wa kahawa, hasa katika kipindi cha masika.
Fedha wanazokatwa, Sh 50 kwa kila kilo moja ya kahawa mnadani Moshi, ilipaswa zikafanye kazi iliyolengwa na sio vinginevyo.
Walishauri waunde mfuko wa pembejeo za kilimo wao wenyewe na makato ya fedha zao, yaelekezwe huko; na si jambo hilo kushughulikiwa na watendaji wa serikali.
Mkulima wa kata ya Ngima, Wilson Kapinga, alisema wanaukataa mfuko huo kutokana na baadhi ya watendaji wa serikali, mabwana shamba, kukosa uaminifu wa kufikisha dawa kwa wakulima. Dawa hizo huishia mikononi mwao na kujinufaisha wao binafsi.
Kapinga alisema maofisa ugani hao, muda mwingi wamekuwa wakiishi mjini badala ya kuwa karibu na wakulima vijijini. Kitendo hicho kinawafanya washindwe kuwajibika ipasavyo, ikiwamo kuwafundisha wakulima utunzaji bora wa mazao yao shambani.
Mkulima mwingine wa kahawa, Peter Komba wa kata ya Myangayanga alisema umefika wakati watendaji hao wachukuliwe hatua za kinidhamu. Kwamba kutowajibika ipasavyo katika maeneo yao ya kazi, liwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.
Mwenyekiti wa MBIFACU wilayani Mbinga, Stanley Lupogo aliunga mkono hoja hizo. Alitaka wakulima wa kahawa kuzalisha zao hilo kwa wingi na kwa ubora unaokubalika katika soko la ndani na nje ya nchi.

Chanzo Gazeti la Habari Leo
 

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa