Home » » BABA WA KAMBO AMUUNGUZA MIKONO MWANYE KWA KUCHELEWA KURUDI NYUMBANI‏

BABA WA KAMBO AMUUNGUZA MIKONO MWANYE KWA KUCHELEWA KURUDI NYUMBANI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


               

Mtoto mmoja wa  miaka nane, mkazi wa Mjimwema Songea mkoani Ruvuma amefanyiwa ukatili wa kutisha na Baba yake wa kambo aitwaye Stan Nyoni kwa kumchoma moto mikono yake yote miwili kwa kosa la kuchelewa kurudi nyumbani.Jeshi la polisi mkoani Ruvuma bado linamsaka mtuhumiwa wa unyama huo,Stan Nyoni ambaye alitoroka baada ya kufanya unyama huo huku mtoto huyo akiwa amelazawa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma Songea.

Tukio hilo la kinyama  limewafanya 

baadhi ya madaktari na manesi wa hospitali hiyo kumwaga machozi kutokana na mtoto Nice kufanyiwa kitendo hicho cha kusikitisha cha kuchomwa moto mikono yake miwili na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake.

Afisa muuguzi msaidizi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma Bw. Aidan Ndunguru anasema mtoto huyo  ameumia katika jicho la kulia,mgongoni huku  akiwa na majeraha makubwa katika viganja vya mikono yake miwili ambayo alimwagiwa mafuta ya taa na kuchomwa moto.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa