MKURUGENZI WA VETA NYANDA ZA JUU ATEMBELEA HOSPITALI YA PERAMIHO MJINI SONGEA

Mkurugenzi wa VETA nyanda za juu,Monica Mbele akiangalia moja ya darubini katika karakana ya vifaa tiba kwenye Hospitali ya St. Joseph Peramiho,wengine ni fundi mkuu wa karakana hiyo Baraka Chumbwi kushoto na katikati kaimu mganga mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dkt Benedict Ngaiza.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya elimu na mafunzo (VETA) nyanda za juu,Monica Mbele akiangalia moja ya vifaa tiba vilivyoharibika katika karakana ya Hospitali ya St Joseph Peramiho,Songea vijijini.VETA ina tarajia kufundisha wataalam na mafundi wa hospitali mbalimbali kutengeza vifaa vilivyoharibika ambapo itasaidia kuokoa kiasi kikubwa cha fedha kwa kuagiza au kuleta mafundi kutoka nje ya nchi kwa ajili ya ukarabati wa vifaa hivyo.
Mkurugenzi wa VETA nyanda za juu,Monica Mbele akiangalia mshine ya kufuria nguo ambayo imeharibika.
Kaimu mganga mkuu wa hospitali ya mkoa wa Ruvuma (homso) Dkt Benedict Ngaiza kulia na mkurugenzi wa VETA nyanda za juu,Monica Mbele wa pili kulia wakiangalia kiti kinachotumika kwa ajili ya shughuli za upasuaji katika hospitali ya St Joseph Peramiho jana.
Fundi mkuu wa karakana ya vifaa tiba katika hospitali ya st Joseph Peramiho Baraka Chumbwiakionesha mojawapo ya mshine ya kupiga picha kwa wataalam na mafundi kutoka chuo cha veta Songea,mafundi kutoka hospitali ya mkoa Ruvuma na ujumbe wa mamlaka ya elimu na mafunzo(veta)nyanda za juu ukiongozwa na mkurugenzi wake Monica Mbele.
PICHA NA MUHIDIN AMRI - GLOBU YA JAMII,RUVUMA.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa