NHIF YAHIMIZA WANAMICHEZO KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


Na Muhidin Amri, Songea.
MFUKO wa taifa wa Bima ya Afya(NHIF) umewahimiza wana michezo nchini kuchangamkia fursa ya kujiunga na mpango wa matibabu kupitia mfuko wa afya ya jamii(CHF) na mfuko wa taifa wa Bima ya Afya(NHIF) kwa ajili ya kupata huduma bora za matibabu pindi wanapoumia wakiwa michezoni.

Rai hiyo imetolewa  mwishoni mwa wiki na meneja wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF)mkoani Ruvuma Abdiel Mkaro wakati wa Bonanza maalum la kuhamasisha jamii hususana wana michezo kujiunga na mfuko huo na kushiriki mazoea mara kwa mara ili kuepuka uwezekano wa kupata magonjwa yasiokuwa ya lazima.

Aliwataka wana michezo na jamii ya watanzania wakiwemo waandishi wa habari,kuona umuhimu wa kijunga na mpango huo  kwa lengo la kuwa na uhakika wa matibabu  pale  inapotokea kupata ajali na magonjwa ya kawaida.

Bonanza hilo liliandaliwa na NHIF lilishirikisha michezo mbalimbali kama vile kukimbia,mazoezi ya viungo,kukimbiza kuku pamoja na mpira wa miguu ambap timu ya soka ya Mkambi FC ilifanikiwa kuibuka mshindi baada ya kuifunga timu ya NHIF 4-2 kwa njia ya Penalti kufuatia matokeo ya kufungana 1-1 ndani ya Dkt 90 za mchezo huo.

Hata hivyo Bonanza hilo lililoonekana kuvutia watu wengi kutoka maeneo mbalimbali ya manispaa ya Songea, baadhi ya washiriki  wameiomba Nhif kuendelea kuandaa bonanza kama hilo kila mwiso wa mwezi ili kutoa fursa kwa wananchi kushiriki na kufanya mazoezi ili kuepusha uwezekano wa kupata magonjwa.

DC ATEMBEZA BAKULI UJENZI WA ZAHANATI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuja Juma Homera kushoto akipokea Cheki ya Shilingi Milioni moja kutoka kwa mkurugezi wa kampuni ya kuuza mafuta ya OIL COM mjini hapa kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa Zahanati ya Kata ya Nakayaya mjini hapa. 

 Na Steven Augustino wa Ruvuma TV Tunduru

 SERIIKALI imewataka wadau mbalimbali wa maendeleo kujitokeza kusaidia ujenzi wa Kituo cha Afya cha Afya Nakayaya Mjini hapa na Kwamba baada ya kukamirika kwa ujenzi huo kituo hicho kitasaidia kupunguza msongamano katika Hospitali ya Serikali ya wilaya ya Tunduru. 

 Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma Juma Homera wakati akipokea msaada wa Shilingi Milioni 1,400,000 kutoka kwa mkurugenzi wa Kituo cha kuuza mafuta cha OIL COM Mjini hapa na kutolewa kwa kwamba msaada huo kutasaidia kukamirika kwa baadhi ya shughuli za ujenzi huo. Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Homera akionyesha Zahanati ya Kata ya Nakayaya ambayo inaendelea kujengwa. Aidha katika taarifa hiyo pia dc Homera ametumia nafasi hiyo kuwapongeza baadhi ya wadau wa maendeleo wa ndani la nje ya wilaya hiyo kwa kujitokeza na kumuunga mkono juhudi za Serikali katika ujenzi wa Kituo hicho kwa lengo la kuwasogezea huduma wananchi.

 Alisema pamoja na michango hiyo kutoka kwa wadau pia serikali inatengeneza utaratibu wa kuwashirikisha wananchi katika ujenzi huo ili nguvu kazi watakayo itoa iweze kusaidia kupunguza gharamaa za ujenzi.

 Tayali ujenzi Zahanati hiyo umekwisha anza na kukamilisha jengo la Utawala katika kituo hicho na kwamba hadi kukamilika kwa ujenzi wa majengo yote 8 yaliyopangwa kughalimu zaidi ya shilingi 419. Akizungumzia tukio hilo Mkurugenzi wa Kituo cha mafuta Cha OIL COM Bw. Ghulam Kalamal alisema kuwa msaada huo ni sehemu ya kampuni yake kurudisha faida iliyopata kutokana na biashara hiyo ili iweze kuhudumia jamii katika eneo hilo. 

 Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Goerge Chiwangu amesema kuwa zaidi ya Wagonjwa wanje 100 hufikana kupatiwa matibabu kwa siku huku kukiwa na kundi la kaati ya akina mama 15 na 20 ambao hufika hospitalini hapo kwa lengo la kijifungua. Hii hapa Video yake .

VIDEO – TUMEKUSOGEZEA MATUKIO MAKUBWA YALIYOJILI MKOANI RUVUMA NA NJE YA MKOA WA RUVUMA WIKI HII.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kama ulipitwa na matukio ya wiki nzima yaliyojili mkoani Ruvuma na nje ya mkoa wa Ruvuma kuanzia Sep 18 hadi Sep 24, 2017 basi usipate tabu tumekusogezea , Matukio ni haya hapa kazi yako ni kubonyeza hii video uweze kuyafahamu na kuyatazama.

VIDEO – WATU WA WILI WAMEFARIKI DUNIA NA 42 WAMEJERUHIWA KATIKA AJALI YA BUS WILAYA YA NYASA MKOANI RUVUMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Watu wa wili wamefariki dunia na 42 wamejeruhiwa katika ajali ya bus aina ya FUSO lenye Namba za usajili T 606 CTY mali ya kampuni ya kisumapai linalofanya safari zake katika wilaya za Songea na Nyasa MBAMBABAY mkoani Ruvuma.

VIDEO – TUMEKUSOGEZEA MATUKIO MAKUBWA YALIYOJILI MKOANI RUVUMA NA NJE YA MKOA WA RUVUMA WIKI HII.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kama ulipitwa na matukio ya wiki nzima yaliyojili mkoani Ruvuma na nje ya mkoa wa Ruvuma kuanzia Sep 11 hadi Sep 17, 2017 basi usipate tabu tumekusogezea , Matukio ni haya hapa kazi yako ni kubonyeza hii video uweze kuyafahamu na kuyatazama.

MATUKIO MAKUBWA YALIYOJILI MKOANI RUVUMA NA NJE YA MKOA WA RUVUMA WIKI HII.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Kama ulipitwa na matukio ya wiki nzima yaliyojili mkoani Ruvuma na nje ya mkoa wa Ruvuma kuanzia Sep 11 hadi Sep 17, 2017 basi usipate tabu tumekusogezea , Matukio ni haya hapa kazi yako ni kubonyeza hii video uweze kuyafahamu na kuyatazama.

RC RUVUMA ,WATAKAO HARIBU VYANZO VYA MAJI KUKIONA CHA MOTO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dkt Mahenge amewataka viongozi hao kuongeza ulinzi katika maeneo hayo, kwa kuwashirikisha viongozi wa mitaa waozungukwa na vyanzo hivyo.  

HIFADHI YA CHAKULA YA MKOA WA RUVUMA NRFA YANUNUA TANI ELFU 5753 KATI YA TANI ELFU 6 WALIZOPEWA NA SERIKALI KUU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mkoa wa Ruvuma umefikia lengo ya ununuzi wa mahindi waliyopanga kununua katika msimu huu wa mavuno kwa vituo vyote ambayo viliteuliwa rasmi na hifadhi ya chakula ya mkoa.

AFYABANDO KAMPENI KUWAKOMBOA WATANZANIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 
Mtaalam Mwelekezi wa Afyabando-Nordic Foundation Tanzania, Dkt. Respicius Salvatory akiongea na waandishi wa habari Dar es Salaam leo Septemba 3 2017, wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kujishindia kadi ya bima ya Afya ijulikanayo kama ‘AfyaBando’. Kulia ni Afisa Mwandamizi Mipango na Utawala wa Taasisi ya Nordic, Maria Nimrod na Afisa Tehama wa Taasisi hiyo, Dickson Leonard.

Afisa Mwandamizi Mipango na Utawala wa Taasisi ya Nordic, Maria Nimrod akifafanua jambo kwa waandishi wa habari Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kujishindia kadi ya bima ya Afya ijulikanayo kama ‘AfyaBando’. Pamoja naye ni Mtaalam Mwelekezi wa Afyabando-Nordic Foundation Tanzania, Dkt. Respicius Salvatory (wa pili kulia) , Afisa Tehama wa Taasis hiyo, Dicson Leonard Afisa Afya na Teddy Uledi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa