Home » » MAHENGE AAGIZA KILA KATA KUJENGA ZAHANATI MOJA YA KIJIJI

MAHENGE AAGIZA KILA KATA KUJENGA ZAHANATI MOJA YA KIJIJI


Na Godfriend Mbuya
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dr. Binilith Mahenge amesema ameagiza kila kata kujenga zahati moja kwenye kijiji kimoja kila mwaka ili kurahisishia wananchi kupat huduma za afya na kuepuka adhan ya kutembea umbali mrefu tutafuta huduma.

Akizungumza na East Afrika Radio katika  kipindi cha SUPAMIX  Mahenge amesema kama kata ina vijiji vinne basi ndani ya miaka minne itakuwa na zahati kila kijiji, huku akisisitiza kuwa serikali ya mkoa imejipanga vizuri kuhakikisha inatatua matatizo makubwa matatu  suala la elimu, maji na afya.

“Wananchi wanatumia muda mwingi kwenda kwenye maji, wanachukua muda mwingi kwenda kwenye vituo vya afya pia muda mwingi watoto kwenda shuleni hivyo muda mwingi wa kufanya kazi kama ilivyo adhma ya serikali ya ‘Hapa Kazi Tu’ unatumika katika kupata huduma za kijamii jambo ambalo tunataka kuondokana nalo kwa kuelekeza nguvu zetu katika maeneo hayo”- Amesema Mahenge.
Aidha kuhusu namna serikali ya mkoa wake inavyosaidi vijana na wanawake Mkuu huyo wa Mkoa amesema agizo la serikali katika Halmashauri zote nchini kutenga asilimia 5% kwa wanawake na 5% kwa vijana linafanyiwa kazi hivyo makundi hayo yajiunge katika vikundi ili kuweza kupata fedha hizo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa