Home » » DC HOMERA AKAGUA MICHE ZA KOROSHO KWA AJILI YA MSIMU UJAO 2016/17

DC HOMERA AKAGUA MICHE ZA KOROSHO KWA AJILI YA MSIMU UJAO 2016/17

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Mhe. Juma Zuberi Homera,akiwa na baadhi ya wakulima wa Korosho
 Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Mhe. Juma Zuberi Homera,akishiriki kumwagilia miche ya zao la Korosho kwenye vitalu


Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Mhe. Juma Zuberi Homera, jana desemba  27,2016 alikwenda CDC kujiridhisha na uandaaji wa miche za mikorosho kwa msimu mpya wa Kilimo 2016/2017 na hatimaye kuridhishwa na maandalizi ya miche ya mikorosho iko ya kutosha na itaanza kusambazwa Kwa mujibu wa utaratibu wa uendelezaji wa zao hilo.

Lakini pia ametoa maelekezo kwa maafisa elimu. alisema, "maafisa elimu wanapaswa kuhakikisha wana kwenda sambamba katika uzalishaji wa zao hili la biashara wilayani Tunduru kwa upande wa shule za msingi na sekondari kwa kuandaa hekari 5 za mikorosho kila shule maafisa kilimo, watendaji wa Kata na vijiji wanapaswa kusimamia zoezi hili na mbegu hizo watagawiwa bure kama mradi wa EK na kuhusu uzalishaji wa mbegu mwaka huu ni mzuri zaidi ukilinganisha na mwaka jana. 
 
Mfano, kitalu cha CDC kina miche zaidi ya 79,000, kangomba zaidi ya miche 49,000, Mbesa zaidi ya miche 25,000, Nalasi zaidi ya miche 20,000, Namasakata zaidi ya miche 20,000, Misechela zaid ya miche 25,000, Muhuwesi 15000, Majimaji zaidi ya miche 10,000, Namiungo zaidi ya miche 15,000, Nandembo zaidi ya miche 15000, na kitanda zaidi ya miche15000 kazi kwetu wanatunduru mbegu hizi za kisasa zinazaa baada ya miaka 3".

Alisisitiza, "lakini pia ni mbegu bora kuhusu minada mpaka sasa wanunuzi mnada wa 4,5,6, wameshalipa bado kuwafikishia vyama vya msingi baada ya kufanya ukokotozi "TWENDE NA MKOROSHO WANGU UCHUMI WANGU" tusisahau kupanda mazao ya Chakula kama mahindi, mpunga, mihogo nk. Tumuunge mkono Rais wetu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika kuinua kilimo nchini na chenye tija kwa wananchi wanyonge na wa hali ya chini. HAPA KAZI TU mungu ni Mwema"

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa