Home » » MWENGE WA UHURU WAANZA MBIO ZAKE MKOANI RUVUMA

MWENGE WA UHURU WAANZA MBIO ZAKE MKOANI RUVUMA


Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Severin Tossi(kushoto) akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Njombe John Mahali .Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo mkoani Ruvuma katika kijiji cha Ngelenge wilaya ya Ludewa kabla haujaanza mbio zake mkoani Ruvuma.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2012 Kapt.Honest E.Mwanossa akimsaidia kubeba ndoo ya maji Bi .Hilda Ngoya mkazi wa kijiji cha Nkaya wilaya ya Nyasa mara baada ya kiongozi huyo kuzindua kisima cha maji kilichoghalimu Tsh 14.9 milioni.Mwenge wa Uhuru utakuwepo mkoani Ruvuma kwa siku sita.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kapt.Honest E.Mwanossa akifungua jengo la hosteli ya wasichana katika shule ya sekondari ya Mbambabay wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.Picha na Muhidin Amri wa Globu Jamii,Ruvuma.
Picha na Blog ya Issa Michuzi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa