Home » » RADI YAUA SITA, YAJERUHI WAWILI

RADI YAUA SITA, YAJERUHI WAWILI

WATU sita wamefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa baada ya kupigwa na radi katika migahawa miwili inayohudumia wanafunzi wa Chuo Cha Maendeleo na Mifugo (LITA).
Tukio tukio hilo lilitokea juzi jioni usiku wilayani hapa wakati wanafunzi hao wakiwa kwenye mgahawa kwa ajili ya kupata mlo wa jioni
Kwa mujibu wa Ofisa Muuguzi Kiongozi wa Kituo cha Afya Madaba, Oraph Pili, siku ya tukio kulikuwa na mvua iliyoambatana na radi ambayo ilipiga eneo walilokuwapo wanafunzi hao
Alisema radi hiyo mara baada ya kupiga ilisababisha vifo hivyo sita na kuwajeruhi wengine wawili waliokuwapo eneo hilo.
Pili aliwataja waliofariki ni Chesko Luoga, mwanafunzi wa mwaka wa pili, Lucas Mabula (mwanafunzi mwaka wa kwanza) Justin Ngonyani na Edwin Funga, wakazi wa Madaba, Hosana Antony Mkazi wa Mbinga na Eva Chapile mkazi wa Njombe ambao walikuwa wafanyakazi wa migahawa hiyo.
Muuguzi huyo aliwataja waliojeruhiwa ni Beatrice Mhagama  mwanafunzi mwaka wa tatu na Leokadia Fusi mkazi wa Madaba
Alisema majeruhi hao mara baada ya kufikishwa kwenye kituo cha afya Madaba na kuonekana wanahitaji matibabu zaidi walihamishwa kwenye hospitali ya rufaa ya Songea wanakoendelea na matibabu.
Muuguzi huyo alisema hali za majeruhi hao zinaendelea vizuri huku miili ya wanafunzi hao imehifadhiwa hospitali ya rufaa Songea na inatarajiwa kusafirishwa kwenda nyumbani kwao kwa mazishi.
Naye Mkuu wa chuo hicho, Darlington Nkenwa, alisema wamesikitishwa na vifo hivyo vilivyotokana radi iliyosababishwa na iliyoanza kunyesha saa 12 jioni hadi saa 5 usiku.
 Chanzo;Tanzania daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa