Home » » WALIMU WALIOGOMA WATISHWA

WALIMU WALIOGOMA WATISHWA

WALIMU wa Wilaya ya Tunduru, mkoani Ruvuma, walioshiriki kwenye mgomo uliolitikisa taifa, wametishiwa kuchukuliwa hatua za kisheria na hata kuwajibishwa endapo itabainika walishiriki.

Ofisa Elimu wa Wilaya ya Tunduru, Rashid Mandoa, aliiambia Tanzania Daima juzi kuwa walimu hao watachukuliwa hatua za kuwajibishwa kutokana na kukiuka taratibu za kufanya mgomo na watahesabiwa kama watoro katika siku walizoshiriki mgomo huo.

Akifafanua tukio hilo, alisema walimu hao watatakiwa kujutia kitendo hicho kutokana na kupotoshwa na uongozi wa Chama cha Walimu (CWT). Mandoa alisema tayari wamekwishatuma timu ya waratibu elimu kata na makatibu kata kutembelea shule zote wilayani humo, ili kubaini walimu walioshiriki mgomo huo.
Chanzo;Tanzania Daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa