Home » » NHIF YAHIMIZA WANAMICHEZO KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA.

NHIF YAHIMIZA WANAMICHEZO KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


Na Muhidin Amri, Songea.
MFUKO wa taifa wa Bima ya Afya(NHIF) umewahimiza wana michezo nchini kuchangamkia fursa ya kujiunga na mpango wa matibabu kupitia mfuko wa afya ya jamii(CHF) na mfuko wa taifa wa Bima ya Afya(NHIF) kwa ajili ya kupata huduma bora za matibabu pindi wanapoumia wakiwa michezoni.

Rai hiyo imetolewa  mwishoni mwa wiki na meneja wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF)mkoani Ruvuma Abdiel Mkaro wakati wa Bonanza maalum la kuhamasisha jamii hususana wana michezo kujiunga na mfuko huo na kushiriki mazoea mara kwa mara ili kuepuka uwezekano wa kupata magonjwa yasiokuwa ya lazima.

Aliwataka wana michezo na jamii ya watanzania wakiwemo waandishi wa habari,kuona umuhimu wa kijunga na mpango huo  kwa lengo la kuwa na uhakika wa matibabu  pale  inapotokea kupata ajali na magonjwa ya kawaida.

Bonanza hilo liliandaliwa na NHIF lilishirikisha michezo mbalimbali kama vile kukimbia,mazoezi ya viungo,kukimbiza kuku pamoja na mpira wa miguu ambap timu ya soka ya Mkambi FC ilifanikiwa kuibuka mshindi baada ya kuifunga timu ya NHIF 4-2 kwa njia ya Penalti kufuatia matokeo ya kufungana 1-1 ndani ya Dkt 90 za mchezo huo.

Hata hivyo Bonanza hilo lililoonekana kuvutia watu wengi kutoka maeneo mbalimbali ya manispaa ya Songea, baadhi ya washiriki  wameiomba Nhif kuendelea kuandaa bonanza kama hilo kila mwiso wa mwezi ili kutoa fursa kwa wananchi kushiriki na kufanya mazoezi ili kuepusha uwezekano wa kupata magonjwa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa