Home » » RC RUVUMA AKANUSHA TAATIFA ZIANAZOZAGAA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII KUWA MAPIGA MARAFUKU KUITA BABY

RC RUVUMA AKANUSHA TAATIFA ZIANAZOZAGAA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII KUWA MAPIGA MARAFUKU KUITA BABY

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
NA DITHA NYONI    WA RUVUMA TV
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amekanusha taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa amepinga marafuku wananchi wa mkoa wa Ruvuma wasiitane baby.
Tamko hilo amelitoa wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ikulu ndogo ya mkoa wa Ruvuma , hii inakuja baadaya ya taarifa kuzagaa na yenye picha inayoonesha mavazi tofauti na eneo alilokuwa anatoa ujumbe katika shule ya sekondari NASULI na MBAMBA BAY huku ujumbe ukisomeka “marukuku kuitana baby” mkuu wa  mkoa wa Ruvuma.
Inline image 2
Hii ni picha inaonyesha tofauti na mazingira 
Inline image 1Na hii ni picha inaonyesha eneo ambalo mkuu wa mkoa akizungumza na wanafunzi wa NASULI sekondari
Ikumbukwe Novemba 8 mwaka huu, mkuu wa mkoa wa Ruvuma alifanya ziara katika halimashauri ya natumbo katika shule ya sekondari nasuli na kuzungumza na wanafunzi hao, huku kampeni kubwa ili kuwa ni kueneza ujumbe wa kumtaka mwanafunzi wa kike kuvaa maguni manne ambayo ni sare ya shule,joho la maafari,gauni la harusi,na matreniti dress
“ili muweze kufanikisha masomo yenu watoto wakike lazima mvae magauni ili muweze kufanikisha malengo yenu”pia mkuu wa mkoa wa Ruvuma aliongeza kuwa ni marafuku watoto wa kiume na wakike kuitana baby
“msikubali kuitwa baby kwa sababu kukubali kuitwa baby ni chanzo cha kujiingiza kwenye mapenzi,mskubali kuitwa queen we ni mwanafunzi unatafuta maisha na wala usikubali kuitwa mrembo au mzuri alisema Rc MNDEME.
Lengo ya kampeni ni kumsaidia mwanafunzi wa kike aweze kufikia ndoto zake za kielimu na kuweza kufanikisha malengo yake.
Kufatia taarifa hizo mkuu wa mkoa alisema ilikuwa inawalenga wanafunzi wa kike na sio watu wazima kwani taarifa zinazoenezwa na makundi ya watu wachache zinalengo la kupotosha umma hivyo wakazi wa mkoa wa Ruvuma wapaswa kupuuzia
Aidha amewataka wazazi na jamii kwa ujumla kutumia kauli mbiu hiyo ya magauni manne ili iwe chachu kwa wanafunzi wa kike waweze kufanikisha ndoto zake,kwani wanaofanya hivyo hawana nia nzuri wa watoto wa kike 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa