Home » » Serikali Mkoani Ruvuma imetoa mwenzi mmoja kwa Wafugaji wa ng'ombe kuhama mkoani Ruvuma

Serikali Mkoani Ruvuma imetoa mwenzi mmoja kwa Wafugaji wa ng'ombe kuhama mkoani Ruvuma



kundi kubwa la ng'ombe katika poli la hifadhi ya selous
Serikali Mkoani Ruvuma imetoa mwenzi mmoja kwa Wafugaji wa jamii za Kisukuma na Wamang‘ati walioingiza Ng’ombe wao kiholela bila kufuata utaratibu kuondoka Mkoani humo vinginevyo Sheria itafuata mkondo wake ikiwa ni pamoja na kufanyika kwa Oparesheni ya kuwafukuza.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said thabity Mwambungu, wakati akiongea na Viongozi wa Serikali Wilayani Tunduru kutokana ukiukwaji wa taratibu za kuingiza wanyama hao bila kufuata taratibu hali ambayo inaweza kuleta madhala na kuzuka kwa mapigano makubwa baina ya wakulima na wafugaji.

Bw. Mwambungu akatumia nafasi hiyo kumtaka Mkuu wa Wilaya hiyo Bw. Chander Nalicho na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bw.Albert Nehata kusimamia zoezi hilo na kuhakikisha kuwa Watendaji wa Vijiji, Wenyeviti wa Vitongoji, Maafisa tarafa kuhakikisha kuwa wanasimamia kwa nguvu zao zote utekelezaji wa tukio hilo na kwa kiongozi anaye jiona kuwa hata mudu basi aachie dhamana hiyo aliyopewa na Serikali.

Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya madiwani wa halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ililidhia kupokea Ng’ombe elfu kumi tu (10,000) na wafuagaji hao kutengewa maeneo katika kata za Mhuwesi, Masonya na Ngapa lakini cha kushangaza wafugaji hao wamekuwa wakiongezeka siku hadi siku na kuenea katika maeneo yote ya Wilaya hiyo.

Wanachi wa wilaya ya Tunduru wamelalamika kuona wafugaji hao kuendelea kuvamia hadi katika hifadhi ya Taifa ya Selous, na hifadhi zamapori tengefu amabazo hutumika katika bishara ya uwindishaji wa Kitaali zilizopo katika maeneo mbali mbali ya vijiji vilivyo Wilayani humo huku kukiwa na makatazo ya kuwazuwia wanachi kuingia na hata kulima.

Afisa Kilimo na Migfugo wa Wilaya ya Tunduru Bw. Chiza Malando mbali na kukiri kwa uingizaji holela wa mofugo hiyo alisema kuwa hivi sasa Wilaya ya Tunduru imeonekana kuelemewa na wingi wa mifugo hiyo,kwani hadi sasa Wilaya hiyo inakadiliwa kuwa na zaidi ya Ng’ombe 40,000 kutoka kwa wafugaji hao tofauti na malengo ya kuwa na Ng,ombe 10,000 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa