Home » » Kesi za mauaji 37 kusikilizwa

Kesi za mauaji 37 kusikilizwa


Ruvuma
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania kanda ya Songea mkoani Ruvuma imeanza vikao vyake katika vituo viwili tofauti Songea na Mbinga ambapo kesi 37 za mauaji zitasikilizwa.
Msajili wa wilaya mahakama kuu Tanzania kanda ya Songea Wilfred Nyansobera alisema kati ya kesi hizo zitakazosikilizwa zipo ambazo maelezo ya awali na ushahidi utasikilizwa.
Nyansobera alisema kikao cha kwanza kitaendeshwa na Jaji Patricia Fikirini akisaidiana na wakili mkuu mfawidhi wa serikali kanda ya Songea Andikalo Msabila na wakili wa kujitegemea Christandus Komba na Frank Ngafumika.
Alifafanua kuwa katika kikao hicho cha kwanza jumla ya kesi 16 zimepangwa ikiwa 12 zitasikilizwa maelezo ya awali na nne zitasikilizwa ushahidi.
Alisema kikao kingine kitaendeshwa na Hakimu Mkazi Mkuu Wilfred Dyansobera akisaidiana na wakili wa serikali Okoa Mgavilenzi na wakili wa kujitegemea Dickson Ndunguru ambapo kesi 10 zimepangwa ikiwemo nne za wauaji kwa ajili ya kusikiliza ushahidi na sita rufaa za jinai.
Kikao kingine kinaendeshwa Mbinga na Jaji mfawidhi kanda ya Songea Mwanaisha Kwariko ambapo jumla ya kesi 11 zimepangwa ikiwa kesi tano za mauaji zitasikilizwa ushahidi na kwamba kesi tatu ni za rufaa za jinai huku zingine tatu zikiwa ni maombi na rufaa ya kesi za madai.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa