Home » » Wakulima Korosho Walalamikia mfumo wa soko la zao hilo

Wakulima Korosho Walalamikia mfumo wa soko la zao hilo



Ruvuma

WAKULIMA wakorosho wameitaka serikali na wadau wa sekta ya korosho nchini kushughulikia kero zilizo katika mfumo wa soko la zao hilo ili liweze kumnufaisha mkulima na kuongeza tija. 

Hatua hiyo inatokana na zao hilo kushindwa kutoa mchango stahiki kupunguza mzigo wa umaskini kwa wakulima wa zao hilo linalotoa mchango mkubwa katika pato la taifa na kuingiza fedha nyingi za kigeni.

Wakichangia mada ya DHANA YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI iliyowasilishwa katika mkutano wa wadau wa sekta ya zao la korosho baadhi ya wakulima hao ndg Ally Maneno wa Pwani,Nicodemas Wilson wa Lindi na Zainabu Kalikalanje wa Ruvuma wamesema swala la upotevu wa korosho katika maghala ya wanunuzi ni changamoto kubwa ambayo isiposhughulikiwa inakatisha tamaa wakulima.

Wamesema kinachoendelea katika mfumo wa soko la korosho ambapo unyaufu unafikia asilimia 25 ya korosho zinazotunzwa katika maghala ni wizi ambao unsipoangaliwa utaua sekta ya kilimo cha zao hilo hapa nchini.

Kumekuwepo na upotevu wa korosho zinapokuwa katika maghala kusubiri bei ya soko mnadani ambao umekuwa ukichukuliwa kama unyaufu madala ya upotevu ambao unepelekea wahusika kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Kisayansi unyaufu unaoruhusiwa katika zao la korosho ni kati ya asilimia 0.9 kwa kipindi cha mwezi mmoja hadi asilimia 1 kwa kipindi cha miezi sita.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa