Home » » WALIMU WATAKIWA KUCHAPA KAZI.

WALIMU WATAKIWA KUCHAPA KAZI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
BAADA ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijijini kufanya vibaya katika matokeo ya kumaliza elimu ya msingi mwaka 2015 kwa kushika mkia mkoani Ruvuma, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Sigsbert Kaijage amewataka walimu kuongeza bidii katika ufundishaji ili kuondoa aibu hiyo kubwa.
Mbali na hilo, Kaijage aliwataka wanafunzi, walimu, wazazi na walezi wilayani humo kushirikiana ili kuinua kiwango cha taaluma kwa lengo la kufikia malengo ya Mpango maalum wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).
Kaijage alitoa mwito huo hivi karibuni wakati akizungumzia kufanya vibaya kwa shule za halmashauri hiyo jambo lililoitia aibu kubwa kwa kuwa ni mara ya kwanza Halmashauri ya Wilaya ya Songea kushika mkia.
Alisema iwapo kila mmoja kuanzia mtoto, mwalimu na mzazi watachukua hatua stahiki na kila mmoja kutimiza wajibu wake itasaidia kufikia kwa malengo yaliyoelekezwa na serikali badala ya jukumu hilo kuliachia serikali.
Kaijage aliwataka wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kutumia muda mwingi kwa ajili ya kujisomea na kuepuka kushiriki katika vitendo vibaya vinayoweza kuchangia kukatisha ndoto za maisha yao.
 CHANZO : HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa