Home » » MBINGA WATAKIWA KUCHANGAMKIA NHIF

MBINGA WATAKIWA KUCHANGAMKIA NHIF

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) amewataka wajasiriamali mkoani Ruvuma kuchangamkia mpango maalumu wa matibabu wa Kikoa waweze kuhudumiwa kwa gharama ya Sh 90,000 kwa mwaka.
Ofisa Mwandamizi wa mfuko huo mkoani Ruvuma, Calytus Mpangala aliwaambia wajasiriamali kutumia fursa hiyo adimu iliyotolewa na serikali kupitia NHIF wawe na uhakika wa kupata huduma bora za matibabu bila kutumia fedha ya mfukoni.
Mpangala alikuwa akizungumza na wateja wa Benki ya Wananchi Mbinga (MCB) katika Wilaya ya Nyasa waliojiunga katika vikundi vya ujasiriamali.
Alisema NHIF inahamasisha wananchi waliopo katika vikundi maalumu vya kiuchumi kama vile vikundi vya kilimo, mama lishe, migahawa na vinginevyo kuchangia Sh 96,000 ambayo Sh 78,600 inakwenda bima ya afya.
Zilizobaki ni kwa ajili ya shughuli za uendeshaji, riba na gharama za wafuatiliaji ambao ni MCB ambao ni mawakala wa NHIF.
Mpangala alisema, kiasi hicho cha fedha kitamwezesha mwana kikundi kupata matibabu kuanzia kwenye zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya na mkoa na hata hospitali ya rufaa popote nchini pale mwanachama wa mfuko huo atakapohitaji kutibiwa, isipokuwa baadhi ya gharama kama usafiri, malazi na chakula zitakuwa za mwanachama mwenyewe.
Chanzo Gazeti la Habari leo
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa