Home » » Mbinga kutumia ziwa Nyasa kuongeza mapato

Mbinga kutumia ziwa Nyasa kuongeza mapato


Mussa Mwangoka, Mbinga-Ruvuma yetu

UONGOZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma umejiwekea  mikakati  kamambe  ya kuongeza makusanyo ya halmashauri hiyo katika mwaka ujao wa fedha kwa kutumia vyema rasilimali zinazotokana na ziwa Nyasa na kuaanisha   vyanzo kadhaa vya kukusanya kodi.

 Akizungumza katika kikao cha pamoja baina Kamati ya Fedha  na Wataalamu wa Halmashauri hiyo katika ziara yao ya siku nne mkoani Rukwa, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo , Oddo Kiliani Mwisho alisema kuwa  wametumia muda mwingi kujifunza katika eneo la Ziwa Tanganyika mkoani Rukwa  na kubaini dosari kadhaa zilizokuwa zikisababisha kupungua kwa pato la halmashari yao.

 “Baada ya  kufanya  ziara  mkoni Rukwa hususani  katika maeneo  ya  mwambao  mwa  Ziwa Tanganyika tumebaini  dosari  kadha wa kadhaa  ambazo   zimekuwa  zikisababisha  kupungua  kwa pato  katika  Halmashauri  yetu  ya Mbinga” alisema Mwisho

Kwa mujibu  wa  Mwisho ufuatia ziara yao mkoani Rukwa wamebaini kuwa kuna vyanzo vingi vya mapato ambavyo wamekuwa wakivipoteza kwenye Ziwa Nyasa hivyo watatumia maarifa waliyoyapata na kuweka mikakati ya kuboresha ukusanyaji wa mapato kwenye ziwa hilo kama zinavyonufaika Halmashauri za Wilaya ya Sumbawanga na Nkasi kwenye Ziwa Tanganyika.

 Alisema  licha ya kuwa  Halmashauri hiyo ya Mbinga  imeweza kuvuka lengo la ukusanyaji wa mapato kufikia zaidi ya  Sh bilioni 1.8 katika mwaka huu wa fedha unaokwisha lakini bado wanayo nafasi ya kuongeza pato la halmshauri hiyo iwapo watatumia fursa zilizopo kwenye  Ziwa  Nyasa.



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa