Home » » MSAFARA WA WAZIRI WA MAENDELEO UVUVI NA MIFUGO WAPATA AJALI

MSAFARA WA WAZIRI WA MAENDELEO UVUVI NA MIFUGO WAPATA AJALI

Dereva wa Shirika la Umeme TANESCO Tawi la Songea, anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kusababisha ajali katika Msafara wa Waziri wa Maendeleo Mifugo na  Uvuvi Dr David Mathayo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsmeki ameyasema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Ajali ilyotokea kutoka Mbambabay – Songea na kusababisha watu 5 kujeruhiwa ambao walilazwa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma.

Akimtaja Dereva anayeshikiliwa na Polisi amesema ni Ahamadi Hamisi 33 ambaye alikuwa akiendesha Gari lenye lenye No. za Usajili SU 37788  TOYOTA Hilax iliyoigonga gari no stk 9906 mali ya RAS Mkoa wa Ruvuma Akiwataja waandishi wa habari walio pata ajali na kulazwa ni   Joseph Mwambije, Lauf Mohamed, Lauf Mohamed, Cresensia Kapinga na Joicy Joliga na mwingine ni Abiria mmoja aliyekuwa kwenye Gari la TANESCO.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsmeki amesema Madereva wa Shirika la TANESCO  Mkoani Ruvuma pamoja na kupewa onyo wamekuwa wakiendelea kwanda kwa  mwendo kasi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsmeki amesema Madereva wa Shirika la TANESCO ambao huendesha kwa kasi gari zao, mara nyingi wapitapo mitaani wamekuwa wakizomewa na Wananchi ikiwa ni ishara ya kupinga mwendo mkali lakini hata hivyo wao huishia kuongeza mwendo . 

Dereva Ahamad Hamis anayeshikiliwa na Polisi anahojiwa na upelelezi utakapokamilika atapelekwa Mahakamani.  

Waziri wa Maendeleo, uvuvi na Mifugo Dr. David Mathayo alikuwa Ziarani Mkoani Ruvuma kwa kutoa Majibu ya Utafiti juu Samaki waliokuwa wanakufa Ovyo katika Ziwa Nyasa Wilayani Nyasa na kugundua ilitokana na Uchafuzi wa Hali ya Hewa na siyo Sumu.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa