Home » » Nchimbi apokelewa na malalamiko ya rushwa Ruvuma

Nchimbi apokelewa na malalamiko ya rushwa Ruvuma

Wananchi wa Manispaa ya Songea wamemlalamikia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Dr. Emmanuel John Nchimbi kuhusu vitendo vya Rushwa vinavyofanywa na Jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma.

Wananchi wa Manispaa ya Songea wamesema wanapokuwa na Matatizo ya kufikishana Polisi na wao wanapokubaliana kufuta kesi badala yake Polisi huomba Rushwa ili kesi ifutwe.

Waziri wa Mambo ya Ndani Dr. Emmanuel Nchimbi akijibu hoja hiyo ya Asikali police kuomba rushwa ili kesi ifutwe amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haikubaliani na vitendo vya Hujuma, mpaka sasa Serikali kwa mwaka 2013 imeshafukuza Askari police 117 waliobainika kuwa na Makosa.

Wananchi wakiwa katika Mkutano wa Hadhara Eneo la Mahenge Kata ya Mjini wameomba Serikali kudhibiti vitendo vinavyofanywa na Jeshi la Polisi. Pia walimlalamikia Waziri kuhusu Uchafu uliokithiri katika Manispaa ya Songea,

Waziri wa Mambo ya Ndani amesema  Manispaa Songea imeshaagiza Magari Mawili ambayo yatasaidia kupunguza kuzoa takataka zilizopo katika Maghuba.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa