Home » » Kichanga kilichotupwa kipo hai

Kichanga kilichotupwa kipo hai

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

HUYU ni mtoto aliyetupwa na mama yake mara baada ya kujifungua katika eneo la Mkuzo manispaa ya Songea mkoani Ruvuma hivi karibuni.Mama mzazi wa mtoto huyo anadaiwa kumtupa huku amemuhifadhi ndani ya mfuko kisha yeye kukimbia.Wasamaria wema walimuokota mtoto huyo akiwa hai na kumpeleka katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma HOMSO  ambako anaendelea kulelewa na kupata huduma zote muhimu kwa mtoto mchanga.
Wauguzi wa hospitali ya mkoa wa Ruvuma  wamempa jina la Thomas huku wakiendelea kutoa malezi bora kwa mtoto huyo ambaye alizaliwa akiwa na uzito pungufu.Hata hivyo mtoto anaendelea vizuri katika wodi ya wazazi na uzito wake unaongezeka .Hapana shaka mtoto Thomas akitimiza uzito unastahili anaweza kwenda kulelewa katika vituo vinavyolea watoto yatima kama vile kituo cha kulelea yatima cha watawa wa mtakatifu Agnes Chipole Songea.
Tabia ya wasichana na wanawake kujifungua kisha kuwatupa watoto wao inaonekana kuendelea kuwa sugu katika maeneo mbalimbali nchini.Mtoto Thomas anahitaji msaada kwa kuwa hafahamiki hadi sasa mama yake wala baba yake, kama umeguswa na unapenda kumsaidia mtoto huyu mahitaji muhimu kwa watoto unaweza kutembelea wadi ya wazazi katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma ama wasiliana nami kwa  baruapepe albano.midelo@gmail.com,au piga simu 0784765917.
Chanzo;Kwanza jamii

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa