Home » » MHAGAMA ; TEHAMA ITAONDOA TATIZO LA WALIMU, VITABU

MHAGAMA ; TEHAMA ITAONDOA TATIZO LA WALIMU, VITABU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WADAU wa elimu wamekubali kutumia teknolojia ya habari na mwasiliano kufundisha na kujifunza ili kukabili tatizo la uhaba wa walimu na vitabu linalokwaza maendeleo ya elimu nchini.
Hayo ni baadhi ya maazimio yaliyotokana na mjadala wa siku mbili wakati wa kongamano la elimu ulioandaliwa na Taasisi ya Learning InSync International kwa kushirikiana na British Council na kufanyika mjini Moshi, Kilimanjaro.
Akizungumza kwenye kongamano hilo, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jenister Mhagama, alisema ili kuharakisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) shuleni, serikali itaongeza kasi ya kuwaelimisha walimu na wanafunzi kuhusu matumizi ya teknolojia itakayorahisishwa na kusambazwa kwa
mkongo wa taifa.
“Pamoja na kukabiliana na mabadiliko ya kiteknolojia duniani, Tehama pia itatuwezesha kuhimili tatizo la uhaba wa walimu na vitabu nchini,” alisema Mhagama na kuongeza kwamba mwalimu atatumia kitabu kufundisha wanafunzi wengi kwa wakati mmoja.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa