Home » » RC RUVUMA AWATAKA POLISI KUFUATA MAADILI YA KAZI

RC RUVUMA AWATAKA POLISI KUFUATA MAADILI YA KAZI

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said thabit Mwambungu amelitaka jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma kufuata Maadili na kuheshimu Kanuni, Taratibu na Sheria za Nchi
                  
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu ameyasema hayo wakati Jeshi la Polisi lilipofanya Maadhimisho ya kuukaribisha mwaka 2014 Sherehe zilizofanyika katika Uwanja wa Kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) sherehe zilizotanguliwa na paredi la Kikosi cha kutuliza ghasia.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema Kazi kubwa ya Jeshi la Polisi ni kulinda mali za raia pamoja na kutii mamlaka yaliyopo katika Dola kinyume na hapo nikulidhalilisha jeshi la Police kimaadili.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu amesema sifa ambayo inaliondolea heshima Jeshi la Police heshima  ni kuwa na moyo wa ubinafsi, chuki na visasi visivyo na tija.

Naye Kamanda wa polisi anayehamia Manyara Deusdedit Nsmeki amesema katika kuukaribisha mwaka 2014 Jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma linajivunia kwa asilimia 75% kupunguza ujanji na kuweza kukamata nyara za serekari pia kuwa karibu na wananchi

Kamanda wa Polisi Deusdedit Nsmeki amesema jambo lingine la kujivunia ni kupungua kwa ajali za barabarani kutoka maelfu ya ajali kwa kila mwaka na kubaki katika mamia ya ajali. Jeshi la Polisi litaendelea kutoa Elimu ili kupunguza ajali.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa