Home » » MTUHUMIWA WA MAUAJI YA WATOTO KIZIMBANI

MTUHUMIWA WA MAUAJI YA WATOTO KIZIMBANI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 MTUHUMIWA wa mauaji ya kulipiza kisasi cha kukataliwa kimapenzi, Bonas Mripa (38), amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Tunduru kujibu tuhuma za mauaji ya watoto wawili.

Akiwasomea shtaka hilo la mauaji namba 5/2014 mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo, Felix Nyalada, Mwendesha Mashtaka Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Inspekta Songelael Jwagu, alidai kuwa mtuhumiwa huyo alifanya kosa hilo Agosti7, mwaka huu kwa kuwaua watoto wawili Vairetih Nilai (8) na mdogo wake Cosmas Nilai (5).

Inspekta Jwagu alidai kuwa mtuhumiwa huyo anadaiwa kula njama na kuua watoto hao baada ya kuvamia nyumba walimokuwa wakiishi na kuichoma moto wakati walipokuwa wamelala saa 7 usiku.

Inspekta Jwagu alidai kwamba, kosa hilo ni kinyume cha kifungu namba 196 sura ya 16 cha kanuni ya adhabu kama ilivyofanyiwa mabadiliko mwaka 2002.

Hata hivyo, mtuhumiwa huyo hakutakiwa kujibu shtaka hilo kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo. Kwa mujibu wa Inspekta Jwagu, upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na mtuhumiwa alirejeshwa rumande hadi Agosti 22, mwaka huu kesi inakapotajwa tena.

Taarifa za awali kuhusiana na tukio hilo zinaeleza kuwa, chanzo cha mauaji hayo ni kulipiza kisasi baada ya mtuhumiwa kukataliwa kimapenzi na mama wa watoto hao

Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa