Home » » POLISI RUVUMA WADAIWA KUMPIGA RISASI DEREVA

POLISI RUVUMA WADAIWA KUMPIGA RISASI DEREVA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Polisi Mkoa wa Ruvuma imeingia matatani baada ya askari wake kudaiwa kumpiga risasi dereva wa bodaboda, Sallgo Nduguru (22) na kumjeruhi kiganja na paja la mguu wa kushoto.
Inadaiwa kuwa, dereva huyo alifikwa na mkasa huo baada ya kutaka kumpora silaha mmoja wa askari waliomkamata kwa kosa la usalama barabarani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, ACP Mihayo Msikhela alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi ili kutuliza ghasia zilizotokea baada ya madereva wengine wa bodaboda kutaka kupambana na askari.
Kamanda Msikhela alisema kuwa tukio hilo lilitokea saa 12 jioni katika eneo la Kombezi, Mfaranyaki, Manispaa ya Songea na kudumu kwa muda wa dakika 30.
Kwa mujibu wa Kamanda Msihkela, askari polisi wawili waliokuwa doria walimkamata kijana aliyetambulika kwa jina moja la Aggrey kwa kosa la kuvunja sheria za usalama barabarani, lakini dereva huyo alimpigia simu mmiliki wake, Sallgo Nduguru ambaye naye ni dereva wa bodaboda na kuja na kundi la madereva wengine.
“Baada ya mmiliki huyo kufika na madereva wengine walianzisha vurugu, ambapo Nduguru alidaiwa kutaka kumpora mmoja wa askari hao silaha,” alisema.
 Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa