Home » » WAKULIMA WATAKIWA KUJIUNGA NA VIKUNDI

WAKULIMA WATAKIWA KUJIUNGA NA VIKUNDI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAKULIMA mkoani Ruvuma wameshauriwa kujiunga kwenye vikundi ili waweze kukopa zana za kisasa za kilimo yakiwemo matrekta aina Power Teller, mashine za kisasa za kupukuchua mahindi ili kuweza kuongeza tija uzalishaji kwani kilimo ni biashara hivyo kuweza kujiongezea kipato.

Ushauri huo ulitolewa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Bapt Company Mkoa wa Ruvuma, Ayoub Mbilinyi ambayo inajishughulisha na uuzaji na usambazaji wa zana za kisasa za kilimo alisema ili wakulima waweze kuzalisha mazao kwa wingi wanapaswa kubadilisha kilimo chao na kulima kilimo cha biashara kwa kutumia zana za kisasa za kilimo.

Mbilinyi aliongeza kuwa kampuni hiyo inatoa mkopo kwa vikundi na mwananchi mmoja moja ambapo wanachoangalia ni vyanzo vyake vya mapato lakini kwa mkulima anaweza akatoa asilimia 70 ya malipo ya awali ambapo kiasi kinachobakia atalipa kulingana na makubaliano maalumu watakayokubaliana au baada ya mavuno ambapo zana hizo zinapatikana wakati wote ambapo mteja akitoa oda yake anapatiwa zana hizo ndani ya siku saba.

Alisema wakulima hao wanaweza kujiunga na kukopa matrekta makubwa 45hp-95hp(4WD) kwani ni imara na zina nguvu na zinatumia mafuta kidogo badala ya kung'ang'ania kutumia jembe la mkono kwani limeshapitwa na wakati.

"Bado mkoani Ruvuma wakulima hawana mwamko wa kutumia zana za kisasa za kilimo nawashauri wakulima wabadilike na kuanza kutumia zana za kisasa za kilimo kwani mbali na kuuza pia tunakopesha vifaa mbali mbali vya kilimo matrekta, powertiller aina ya Maize Thresher kwa bei nafuu kwani mkulima anaweza kununua kwa kiasi cha sh. milioni 5.5, mashine za kisasa za kupukuchulia mahindi, mashine za kupanda mpunga; na kuvunia mpunga, mashine za kuvuna ngano pamoja na pampu za kumwagilia maji ambapo matarajio yao ni kuhakikisha wanasambaza pembejeo za kilimo zikiwemo dawa,mbolea pamoja na mbegu," alisema.

Aidha, aliwashauri wakulima wa Mkoa wa Ruvuma kununua vipuri vya matrekta mbali mbali ambavyo havipatikani mkoani humo kwenye kampuni hiyo.

Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa