Wasafirishaji Ruvuma wadai mil. 375/-

na Stephano Chitete, SongeaWASAFIRISHAJI wa mizigo mkoani Ruvuma, wameitaka Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika kuona umuhimu wa kuwalipa deni lao la sh milioni 375 wanazozidai kwenye kitengo cha Taifa cha kuhifadhi mahindi kilichopo (SGR).Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wasafirishaji hao ambao wameomba majina yao yahifadhiwa, walisema kuwa walikopwa kuyasafirisha mahindi hayo kwa ahadi kuwa fedha zao wangelipwa mara baada ya kumaliza kazi lakini hadi sasa hawajalipwa.Walisema kuwa wafanyabiashara wengine waliikodisha serikali magodauni ili wahifadhi mahindi hayo kwa sababu yale ya kituo cha hifadhi kilichopo mjini hapa hayakuwa na uwezo wa kumdu mahindi yote.Walisema kuwa walijitahidi kwa uaminifu mkubwa kufanya kazi hiyo ya kubeba mahindi kutoka kwenye maeneo ambayo...

Kampuni kufundisha wakulima 100,000 shamba darasa

Mwandishi Wetu, SongeaKAMPUNI ya Lutukira Mixed Farm Project  yenye makao yake jijini  Dar es Salaam imepanga kutoa mafunzo ya shamba darasa kwa wakulima 100,000 watakaozunguka eneo la mradi wa  uwekezaji wa kilimo  cha karanga,ufuta  na alizeti  wilayani Songea. Mradi huo tayari umepata eneo la ekari 20,000 za kulima mazao ya kibiashara na kujenga kiwanda cha kukamua mafuta ya mbegu. Wakulima watakaofundishwa watalima mazao mbalimbali na kuyauza kwenye kampuni hiyo ambayo itayakamua na kuyaunza nje ya nchi.  Mwenyekiti ambaye pia ni  Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni  hiyo, Alhaji Said Kilahama alisema hayo jana jijini hapa alipozungumzia mkakati ya kutekeleza mradi wa kilimo Lutukira Mixed Farm Project.Alisema  mafunzo hayo yatatolewa katika...

Mwandishi MCL ahukumiwa kwa rushwa

Mwandishi Wetu, Songea MWANDISHI wa Gazeti la Mwananchi mkoani Ruvuma, Kwirunus Mapunda amehukumiwa kwenda jela miaka sita au kulipa faini ya Sh 1,000,000 baada ya kukutwa na hatia ya makosa mawili ya kuomba na kupokea rushwa kutoka Shirika la Watawa Wabenediktine la Peramiho.  Mapunda ametiwa hatiani na Mahakama ya Wilaya ya Songea wiki iliyopita chini ya Hakimu Mfawidhi wa Wilaya hiyo, Elizabeth Misana. Mwendesha Mashitaka wa Takukuru, Christa Kabekenga alidai kwamba Mapunda alitenda kosa hilo Desemba mwaka jana kwa kuomba rushwa ya Sh2 milioni ili asiandike habari mbaya za shirika hilo la Wabenediktine, lililo chini ya Kanisa Katoliki Jimbo Kuu Songea.  Ilidaiwa kwamba baada ya kuomba kiasi hicho uongozi wa shirika hilo ulitoa taarifa Takukuru ambayo ilimwekea mtego na kumnasa.  Akisoma...

Mgogoro wa ardhi wamalizika

Na Amon Mtega, SongeaMGOGORO wa ardhi kati ya wananchi wa Kijiji cha Lutukila, Kata ya Mkongotema, Songea Vijijini na mwekezaji wa shamba la Kampuni ya Lutukila Mixed Farm umekwisha, baada ya mwekezaji huyo kukubali kukaa meza moja na wanakijiji hao kwa kukubaliana masuala ya msingi yaliyokuwa yakihitajika kabla ya kusaini mkataba wa umiliki wa shamba hilo. Makubaliano hayo yalifanyika mjini hapa jana, wakati wa mkutano uliofanyika katika kijiji hicho, baada ya wananchi hao kumtaka mwekezaji huyo akubaliane na mahitaji waliyokuwa wakihitaji. Akiwakilisha madai yao, Mwenyekiti wa Kamati ya Kufuatilia Makubaliano, Eligius Danda, alisema mambo wanayotaka wafanyiwe ni maji ya bomba, kuchangia utengenezaji wa barabara ziendazo mashambani, ukarabati wa madarasa ya shule za sekondari na msingi,...

RC awasihi wana Ruvuma kuwakubali wawekezaji

Kwirinus Mapunda, Songea SERIKALI mkoani Ruvuma imewataka wananchi kutowakatisha tamaa wawekezaji wanaofika kwenye maeneo yao kwa lengo la kuwekeza badala yake wawaunge mkono kwa kushirikiana nao ili kuinua hali ya uchumi wao na mkoa kwa ujumla. Akizungumzia hali ya uwekezaji mkoani mwake, Mkuu wa mkoa huo, Said Mwambungu alisema Serikali imekuwa mstari wa mbele kuweka mazingira bora ya kuwavutia wawekezaji mkoani humo na kwamba kinachotakiwa ni kwa wananchi nao kuhakikisha wanatoa ushirikiano ili kufikia malengo yaliyokusudiwa. “Jitihada za Serikali katika kuhamasisha wawekezaji mkoani hapa zinapaswa kuungwa mkono na wananchi wote kwani zitawapa manufaa makubwa,’’ alisema na kufafanua kwamba mkoa huo upo nyuma kwa uwekezaji ukilinganishwa na mikoa ya kaskazini ambapo wawekezaji ni wengi...

Ufunguzi wa soko la Tumbaku Mkoani Ruvuma

Kaimu meneja wa chama cha ushirika cha wilaya ya Namtumbo na Songea(sonamcu) akimkabidhi risala ya wakulima wa chama hicho mkuu wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Abdala Lutavi.Mwenyekiti wa SONAMCU,Awami Ngonyani akizumngumza wakati wa ufunguzi wa soko la Tumbaku katika kijiji cha Matepwende wilayani Namtumbo ,kulia mkuu wa wilaya hiyo Abdala Lutavi.Baadhi ya wakulima wa tumbaku wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma,wakikagua tumbaku yao kabla ya kuuza kwa makampuni yanayonunua tumbaku kwenye ufunguzi wa mauzo ya zao hilo katika kijiji cha Matepwende wilayani humo.Wakulima wa Tumbaku kutoka katika kata ya Lwinga wilayani Namtumbo...

MWENGE WA UHURU WAKIMBIZWA WILAYA YA NAMTUMBO

Mwenge wa Uhuru ukikimbizwa kuingia katika wilaya ya Namtumbo kuanza kazi ya kuhamasisha shughuli za maendeleo ukitokea wilaya ya Songea.Jumla ya miradi  11 yenye thamani zaidi ya shilingi milioni 400 imezinduliwa,imewekewa mawe ya msingi na kufunguliwa. Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kapteni Honest Mwanossa akichanganya mbolea wakati wa uzinduzi wa shamba la michungwa  kwa kutumia  mbolea vunde kwa kuongeza ubora wa mazao na hifadhi ya mazingira katika kijiji cha Msindo wilaya ya Namtumbo.Shamba hilo lenye ukubwa wa hekari mbili na nusu linamilikiwa na Mzee Venant Haule (mwenye fulana nyekundu). Mtoto Mezea...
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa