Home » » MLEMAVU WA KUSEMA NA KUSIKIA AMUUA BABA YAKE MZAZI KWA KUMTANDIKA NA MPINI WA SHOKA.‏

MLEMAVU WA KUSEMA NA KUSIKIA AMUUA BABA YAKE MZAZI KWA KUMTANDIKA NA MPINI WA SHOKA.‏

Kijana wa umri wa Miaka 29 mwenye ulemavu wa kushindwa kuongea (Bubu) aliyefahamika kwa jina la Zuberi Hatima Said anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumuua Baba yake Mzazi  akiwa anamtuhumu kumroga.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Deusdedit Nsimeki amemtaja Marehemu huyo kuwa ni Hatima Said Lung’ande (70) na kwamba katika tukio hilo mtuhumiwa alimuua kwa kumpiga na mpini wa Shoka.
Kamanda Nsimeki aliendelea kufafanua kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 29 /2013 majira ya Saa 12  Jioni katika kitongoji cha Mchangani kilichopo katika Kijiji cha Kazamoyo Tarafa ya Lukumbule Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma.





Alisema kuwa kufuatia hali hiyo mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani ili sharia iweze kufuata mkondo wake baada ya kukamilika kwa taratibu za mahojiano yatakayo washirikisha wataalamu wa Lugha za alama. 

Akizungumzia tukio hilo mkalimani wa familia hiyo Mtoto wa kwanza kati ya watoto wane wa marehemu Lung’ande Bw.Adamu Sadiki alisema kuwa kabla ya tukio hilo ndugu yake huyo ambaye ni kati ya watoto watatu wa marehemu wenye ulemavu huo alidaikuwa kwa muda mrefu amekuwa akimuona marehemu usiku akiwa anamuwangia.

“Tumezaliwa watoto Wanne katika familia yetu kwa Baba na mama Lung’ande lakini kutokana na mipango ya mungu wenzangu wote ni mabubu hivyo mimi nimekuwa kiunganishi kikubwa katika familia, wageni pamoja na ndugu na jama” alisema Bw. Adamu na kuongeza kuwa Zuberi amekuwa akimlalamika baba kuwa ni mchawi siku za hivi kalibuni hali ambayo iliwaweka katika mazingira ya utata miongoni mwao.


Mganga aliye ufanyia uchunguzi mwili wa Marehemu Lung’ande, Dkt. Joseph Ng’ombo alisema kuwa kifo hicho kilisababishwa na tukio la kutokwa na damu nyingi kufuatia kipigo hicho. Alisema katika tukio hilo marehemu aliumia vibaya Kichwani upande wa jicho la kulia pamoja na kupasuka kwa fuvu la kichwa chake na jicho la Kulia kufutia kipigo hicho.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa