Home » » Tunduru yapitisha bajeti YA MAENDELEO

Tunduru yapitisha bajeti YA MAENDELEO

HALMASHAURI ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma imepitisha bajeti ya zaidi sh.bilioni 40.3 kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya kawaida ikiwa ni pamoja na kutekeleza miradi ya maendeleo kwa mwaka 2014/15.
Akisoma taarifa ya mapendekezo ya mpango wa bajeti ya halmashauri hiyo,Ofisa
Mipango wa halmashauri hiyo, Kenneth Haule, alisema halmashauri hiyo inatarajia kukusanya zaidi ya sh.milioni 134.7 kutoka katika vyanzo vyake vya mapato kwa ajili ya miradi ya maendeleo na matumizi ya kawaida mishahara na mengineyo sh.bilioni 25.3.
Alisema, bajeti hiyo imeongezeka kwa sh. bilioni 4.5 ambapo wanatarajia zaidi kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuweza kuongeza mapato ya halmashauri hiyo.
Akichangia wakati wa kikao hicho Mbunge wa Jimbo la Kusini, Abdallah Mtutura, aliwataka madiwani kusimamia mapato kwani wao ndiyo wanaojua namna mapato yanavyovuja kwani wao ndiyo wanaoishi na wakusanya ushuru. Aliwataka madiwani hao wasimamie pia matumizi ya fedha walizokusanya ikiwa ni pamoja na kuacha kufanya siri bali wawafichue wanaohujumu mapato ya halmashauri hiyo

Chanzo;Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa