Home » » TATIZO LA UKOSEFU WA UMEME RUVUMA KUMALIZIKA MWAKA 2015

TATIZO LA UKOSEFU WA UMEME RUVUMA KUMALIZIKA MWAKA 2015

Mkoa wa Ruvuma unatarajia kuondokana na tatizo la umeme ifikapo mwaka 2015 baada ya mradi wa umeme kutoka Luli Chipole kukamilika na kuweza kutoa MG 8 ambazo zitasaidia kusambazwa katika Wilaya ya Mbinga, Nyasa na Songea.

Naibu Mkurugenzi wa TANESCO Bonifance Njombe ameyasema hayo alipokuwa akiongea na Waandishi wa Habari kuelezea kero ya umeme inayoukabili Mkoa wa Ruvuma.

Naibu Mkurugenzi amesema mahitaji halisi ya umeme kwa Mkoa wa Ruvuma ni MG 4.3 lakini kwa sasa umeme unaopatikana ni MG 1.6. Jambo linalosababisha kuwepo kwa mgao. Amesema hayo yote yanatokana na kuharibika kwa Mashine 3 zinazosambaza umeme katika Manispaa ya Songea.

Naibu Mkurugenzi wa TANESCO Bonifance Njombe amesema kutokana na jitihada za Shirika la umeme Mashine mbili zimeshatengenezwa na kuweza kupunguza kero za mgao wa umeme, Mashine ya mwisho ikishapona itasaidia kuwa na umeme wa ziada KW 400.

Naibu Mkurugenzi wa TANESCO amesema mashine zinazotumia maji za chipole zikikamilika zitaweza kutoa MG Wat 8 wakati Matumizi ya Chipole ni MG 1 moja tu jambo litakalouwezesha Mkoa wa Ruvuma kuwa na Migawat 14 ambazo zitasambazwa wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa