Home » » Chadema yawaonya wanaochafuana

Chadema yawaonya wanaochafuana

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa amewaonya baadhi ya wanachama wanaochafuana na waliojitokeza kutangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali za udiwani, ubunge kabla ya wakati akiwamo mwenyekiti wa chama hicho mkoani hapa, Joseph Fuime.
Mwenyekiti huyo anadaiwa kutangaza nia ya kugombea ubunge wa Jimbo la Songea mjini na kutakiwa kuacha mara moja, kabla ya hatua kali za kinidhamu hazijachukuliwa dhidi yao kama kanuni ya chama hicho inavyosema,ikiwamo pamoja na kufukuzwa uanachama, kusimamishwa au kupewa adhabu zilizopo kwenye kanuni.
Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu jana kuhusu onyo lake Dk Slaa amesema, kutangaza nia siyo dhambi ni haki ya mwanachama na siyo mgogoro ila anapaswa afuatae kanuni za chama zinavyoelekeza na iwapo kanuni zitavunjwa na mgombea basi hawatasita kumchukulia hatua.
“Ni kweli kuna baa dhi ya wanachama wanatangaza nia na hawafuati kanuni zinavyosema,tayari chama kimeshapeleka waraka katika majimbo, wilaya na mkoa wasome na kuelewa,iwapo hawajapata waraka huo wawasiliane na ofisi yangu watumiwe kwani wakibainika watapata matizo pamoja na kuchukuliwa hatua za kinidhamu,”alisema Dk Slaa.
Mwenyekiti wa chama hicho Singida, Joseph Fuime hakuweza kupatikana kuzungumzia tuhuma hizo kwani simu zake zote za mkononi hazikupatikana.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa