Home » » VIJIJI VIWILI VYAANZA KUVUNA ASALI KWA WINGI

VIJIJI VIWILI VYAANZA KUVUNA ASALI KWA WINGI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Wananchi wa vijiji vya Mtyangimbole na Gumbiro Songea  Vijijini baada ya miezi miwili  wanatarajia kuvuna kilo 500 za Asali  na Nta kilo 50 baada ya kutundika mizinga 50 katika Msitu wa Hifhadhi
                            
Mkuu wa Wilaya ya Songea Joseph Joseph Mkirikiti akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabiti Mwambungu amesema hayo katika wiki ya kitaifa ya kutundika mizinga iliyo fanyika kijiji cha Mtyangimbore .Amesema Mpango wa serekari wa Matokeo Makubwa sasa ni kubuni mipango mbali mbali ya kumwongezea Mwananchi wa Chini kipato kupitia Ufugaji wa Nyuki’

Mkuu wa wilaya ya Songea Joseph Joseph Mkirikiti amesema umefika wakati sasa wa kujenga urafiki na Nyuki badala ya kuwaona Nyuki kama Adui amewataka wananchi kuepuka na  kuchoma misitu ovyo unao sababisha viumbe wengi kutoweka wakiwemo nyuki.

Mkuu wa wilaya ya Songea Joseph joseph Mkirikiti akimwakilisha mkuu wa Mkoa Said thabit Mwambungu amesema Serekari ina buni mbinu mbali mbali kuongeza kipato kwa Mwananchi kupitia Mali asili tulizo nazo nyuki walioko wapatao milioni 9.2 wakitunzwa vizuri wataweza kuongeza hali ya uchumi kukua ikiwa pamoja na kuongeza fedha za kigeni ,Hivyo tabia ya kuangamiza viumbe vyenye kuleta tija iachwe mara moja


Meneja wa Misitu Wilaya ya Songea Manyisye Mpokigwa amesema juhudi za Idara yake kuhusu Utundikaji wa Mizinga na kulinda Misitu sasa inaonyesha mafanikio wananchi wengi wa vijijini wameanza kuvuna Asali .

Naye Mwakilishi wa Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania Gaudens Kilasi amesema kutokana na Mizinga 25 iliyotolewa mwaka jana na mizinga 25 ya sasa itawasaidia wananchi kuvuna Tani 500 za Asali swala litakalo saidia kupunguza umasini kwa wananchi wa vijijini.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Joseph joseph Mkirikiti amesema Jumla ya Makundi Milioni 9.2 ya nyuki yapo hatarini kutoweka endapo wananchi hawataacha mtindo wa kuchoma Misitu ovyo, amewaomba Wananchi kuacha kuwa Maadui na Nyuki au Misitu sasa wawe marafiki kwa Nyuki.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa