Home » » CHANGAMOTO ZA USAFIRI RUVUMA ZA PUNGUA

CHANGAMOTO ZA USAFIRI RUVUMA ZA PUNGUA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma wameisifu SUMATRA kwa kuweza kusimamia safari za Mabasi na kufanikisha kupanga safari katika sehemu ambazo zilikuwa ni kero kwa Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma.
                       
Mohamed Chichi akizungumza kwa niaba ya Wasafiri katika Kituo Kikuu cha Mabasi Songea, amesema katika Changamoto zilizokuwa zinawakabili Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma ni kukosa Usafiri wa Songea – Dodoma, Songea – Mwanza na Songea – Mbamba Bay. Njia zote hizo zimefunguka tunaishukuru Serikali kwa kuweza kutatua changamoto hizo.

Afisa Mfawidhi wa SUMATRA Mkoa wa Ruvuma Denis Daudi amesema Mkoa wa Ruvuma una changamoto nyingi za usafiri, Ukiwemo usafiri wa Songea – Mkenda –njia inayo unganisha na Nchi ya  Msumbiji na Tanzania ,na Songea  Tunduru bado kunahitajika Usafiri wa uhakika,

Barabara ya Songea – Mkenda serekali ina fanya mipango ya kumpata mfadhili ili atengeneze njia hiyo  kwa kiwango cha Lami itaweza kufungua mawasiliano kati ya Msumbiji na Tanzania. Amewataka  wananchi kuwa watulivu wakati juhudi za serekali zikitafuta njia ya kutatua changamoto hizo
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa