Home » » WAZABUNI SONGEA WAKUMBUSHIA DENI LAO

WAZABUNI SONGEA WAKUMBUSHIA DENI LAO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WAZABUNI wa vyakula katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea, wameikumbusha serikali kuangalia uwezekano wa kuwalipa deni lao la zaidi ya sh bilioni moja lililotokana na kulisha katika shule za sekondari, vyuo na taasisi mbalimbali mkoani hapa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Tanzania Daima jana, wazabuni hao ambao hawakutaka kutajwa majina, walisema pamoja na ahadi nyingi za viongozi wa kitaifa kutolewa juu ya kulipa madeni hayo, lakini hadi sasa hakuna  utekelezaji.
Walisema mbali ya Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jenista Mhagama, kuwaahidi waendelee na kazi  ya kulisha katika shule na vyuo wakati malipo yao yakishughulikiwa, jambo hilo hadi sasa limekuwa hadithi.
Walisema wamekuwa wakiendesha shughuli ya kulisha kutokana na mikopo inayotolewa kwenye taasisi za fedha, jambo ambalo wamedai hivi sasa limewaweka mahali pabaya kutokana na taasisi hizo kutaka kuuza mali zao kutokana na kuchelewesha marejesho.
Walisema endapo serikali haitaharakisha malipo hayo, watashindwa kuendelea kulisha katika shule hizo, kwani fedha iliyotumwa kwenye baadhi ya shule za sekondari na vyuo kiasi cha sh milioni 72 hazitoshi kwa kugawana wazabuni wote kwani zinatosha kulisha kwa siku 40 tu.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa