Home » » Meja Jenerali Msemwa kuzikwa leo

Meja Jenerali Msemwa kuzikwa leo

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399
<p>MWILI  wa  aliyekuwa  Meja Jenerali  wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ),  Kevin Msemwa, umewasili  mjini Songea  na  kupokewa na viongozi mbalimbali wa  serikali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu.</p> <p>   Mwili  huo uliwasili  jana, saa 4 asubuhi kwa ndege ya jeshi   hilo  katika Uwanja wa Ndege wa  Ruhuwiko  wa mjini Songea na kuelekea  nyumbani kwa marehemu maeneo ya Seed Farm   mjini humo.</p> <p>   Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuwasili kwa  mwili huo, Luteni Jenerali na Mnadhimu wa Jeshi, Samweli Ndomba, alisema  marehemu Msemwa anatarajiwa kuzikwa leo saa 8 mchana katika makaburi ya  Mfaranyaki mjini Songea.</p> <p>   Msemaji wa familia, Nicas Msemwa, alisema kuwa Kevin  alifariki dunia Aprili 3, mwaka huu alipokuwa akipatiwa matibabu katika  Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam.</p> <p>   Nicas ambaye ni mdogo wa marehemu, alisema misa ya mazishi  itafanyika katika Kanisa Kuu la Kiaskofu la Mtakatifu Mathias Mulumba Kalemba,  mjini Songea.</p>MWILI  wa aliyekuwa  Meja Jenerali  wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Kevin Msemwa, umewasili  mjini Songea na  kupokewa na viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu.
Mwili  huo uliwasili jana, saa 4 asubuhi kwa ndege ya jeshi  hilo  katika Uwanja wa Ndege wa Ruhuwiko  wa mjini Songea na kuelekea nyumbani kwa marehemu maeneo ya Seed Farm  mjini humo.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuwasili kwa mwili huo, Luteni Jenerali na Mnadhimu wa Jeshi, Samweli Ndomba, alisema marehemu Msemwa anatarajiwa kuzikwa leo saa 8 mchana katika makaburi ya Mfaranyaki mjini Songea.
Msemaji wa familia, Nicas Msemwa, alisema kuwa Kevin alifariki dunia Aprili 3, mwaka huu alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam.
Nicas ambaye ni mdogo wa marehemu, alisema misa ya mazishi itafanyika katika Kanisa Kuu la Kiaskofu la Mtakatifu Mathias Mulumba Kalemba, mjini Songea.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa