Home » » DC TUNDURU AMPONGEZA MWEKEZAJI

DC TUNDURU AMPONGEZA MWEKEZAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MKUU wa Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, Chande NalichoMKUU wa Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, Chande Nalicho, amempongeza Mwekezaji wa nyumba ya kulala wageni ya Peramiho, Faustin Chale kwa uwekezaji alioufanya wilayani hapo.
Alisema ujasiri wa mwekezaji huyo wa kutumia mkopo wa sh milioni 100 kwa ajili ya mradi wa nyumba hiyo ni jambo jema alilodai kuwa litapunguza adha ya malazi kwa wageni wakati wa sherehe za kimkoa na ziara za viongozi wa kitaifa.
Nalicho alisema hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima huku akiwataka wananchi wengine kuiga mfano wa mdau huyo wa maendeleo.
Alisema mwekezaji huyo mzawa ni mtumishi wa serikali hivyo anastahili pongezi kwa aina hiyo ya uwekezaji wa gharama kwa ajili ya shughuli za maendeleo huku wengine wakiogopa kukopa na kuwekeza wilayani humo kwa madai ya miundombinu mibovu ya barabara.
Aliwataka watumishi wa serikali kutumia fursa ya kufunguka kwa barabara kutoka Mtwara kupitia Tunduru na kutoka Tunduru hadi Songea itakayojengwa kwa kiwango cha lami mapema mwaka huu kujiwekea vitega uchumi vitakavyowasaidia baada ya kustaafu.
Kwa upande wake mmiliki wa nyumba hiyo, Faustin alisema asili ya mafanikio na maendeleo yake ni kukopa hivyo amewashauri watumishi wengine nao kuandaa maisha yao kwa kuweka vitega uchumi badala ya kutegemea fedha za kiinua mgongo.
Mradi huo ulifunguliwa na kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa, Rachel Kassanda wakati mwenge huyo ulipopita wilayani Tunduru mwishoni mwa wiki.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa