Home » » 'MSIHIFADHI WAHAMIAJI HARAMU'

'MSIHIFADHI WAHAMIAJI HARAMU'

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
KIONGOZI wa mbio za mwenge wa uhuru, Rachel Kassanda, amewataka Watanzania kuacha tabia ya kuwahifadhi wahamiaji haramu, kwani kwa kufanya hivyo ni kuhatarisha amani na usalama wa nchi.
Akizungumza baada ya kuzindua nyumba ya Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Ruvuma, Kassanda aliwalaumu wakazi wa maeneo mbalimbali ya mpakani mkoani hapa kwa kuiweka rehani amani na usalama wa nchi bila sababu za msingi.
Alisema uhamiaji pekee haiwezi kufanya kazi bila kushirikiana na wananchi, hivyo wanapaswa kusaidia kwa kutoa taarifa muhimu za kiuhamiaji na kuwezesha udhibiti matukio ya kihalifu.
Alisema mkoa huo ndio mapitio ya makundi ya wahamiaji haramu kutoka Ethiopia na Somalia wanaoelekea kusini mwa Afrika, hivyo wananchi wakitoa msaada kwa maofisa wa uhamiaji wanaweza kukomesha hali hiyo.
Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Ruvuma, Koku Lwebandiza, aliishukuru serikali kwa kuwezesha kujengwa kwa nyumba hiyo ambayo  imegharimu sh milioni 434.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa