Home » » WAFANYABIASHARA WAKATAA KUKATWA 20

WAFANYABIASHARA WAKATAA KUKATWA 20

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
WAFANYABIASHARA wa kampuni za ununuzi wa kahawa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Ruvuma, wamekataa kuendelea kukatwa sh 20 kwa kila kilo ya zao hilo kuchangia mfuko wa ununuzi wa dawa za kuthibiti vidung’ata.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Tanzania Daima Jumatano, baadhi ya wafanyabiashara hao (majina yamehifadhiwa) walidai kuwa fedha zinazokatwa kwa ajili ya kuchangia mfuko huo zinatumika kwa manufaa ya wajanja wachache kwa sababu ugonjwa huo umetoweka miaka mitatu iliyopita.
Walisema fedha zilipangwa kukatwa kipindi cha dharura kwa ajili ya kulinusuru zao hilo lisishambuliwe na ugonjwa wa vidung’ata, lakini sasa wamegeuza sheria licha ya ugonjwa huo kutoweka.
“Suala linalotakiwa ni kukaa mezani kati ya halmashauri na wafanyabiashara wa kahawa badala ya kutumia ubabe kukata fedha hizo na kufanya urasimu katika utoaji wa vibali vya kununulia zao hilo kwa sisi tunaopinga suala hilo,” alisisitiza mmoja wao.
Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Senyi Ngaga, alisema madai ya wafanyabiashara hao hayana ukweli, badala yake ametaka makato hayo yaendelee hadi ugonjwa huo utakapotokomea kabisa huku akibainisha kwamba baadhi ya maeneo yanasumbuliwa na vidung’ata.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa