Home » » KAMPUNI YA MKULIMA KUNUNUA MPUNGA SONGEA

KAMPUNI YA MKULIMA KUNUNUA MPUNGA SONGEA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
WAKATI Serikali inahangaika kutafuta masoko ya kuuzia mazao ya wakulima, kampuni ya kizalendo ya Mkulima Malt Purpose yenye makao yake makuu jijini Mbeya imejitosa kuanza kununua mpunga.
Kampuni hiyo ambayo kwa sasa inajishughulisha na kilimo cha mpunga katika Kijiji cha Nambendo, wilayani Songea, Ruvuma, imejitolea kuanza kununua mpunga wa wakulima hao kwa lengo la kuwanusuru na tatizo la ukosefu wa soko katika msimu wa 2013/2014, ambako lengo lake ni kununua wastani wa tani 80 zenye thamani ya zaidi ya sh milioni 30.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Hamis Msigwa, alisema tayari wamekwisha nunua tani 16 za mpunga.
Msigwa, alisema kampuni yake imeamua kununua mpunga huo kutokana na wakulima wa kijiji hicho kuongeza uzalishaji wa zao hilo, kutoka wastani wa tani 10 hadi kufikia 80 baada ya kampuni hiyo kutoa elimu juu ya kilimo hicho, ikiwemo kuwagawia mbegu tani tatu kwa wakulima wa vitongoji nane vya kijiji hicho pamoja na kuwalimia mshamba yao bure.
Alisema kuwa, licha ya kuwakwamua wakulima hao kwa kununua zao hilo, kampuni hiyo inatarajia kuboresha  kilimo cha zao  hilo kwa kuongeza jitihada zaidi ya kuwagawia mbegu bora ya mpunga ambayo itakuwa na uwezo wa kuzalisha gunia 30 kwa ekari moja.
Kampuni hiyo inajishughulisha na kilimo cha zao la Mpunga katika maeneo yafuatayo ikiwemo ,Chimala Mbeya,Mtwara vijijini pamoja na Kijiji cha Nambendo kilichopo katika Halmashauri ya wilaya ya Songea vijijini
mkoani Ruvuma.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa