Home » » Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma akabidhi vyeti kwa wahitimu 502 chuo cha Ualimu Songea

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma akabidhi vyeti kwa wahitimu 502 chuo cha Ualimu Songea


 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,Mh. Said Mwambungu akimpongeza mmoja kati ya wahitimu 502 wa Stashahada ya Ualimu wa Chuo cha Ualimu cha Songea mara baada ya kumkabidhi cheti chake,wakati wa mahafali ya 11 ya chuo hicho.
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,Mh. Said Mwambungu akizungumza na Wazazi,Walimu na Wahitimu katika Chuo Cha Ualimu cha Songea.kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho, Bi. Ilolima Lugomi na kulia Mkuu wa Chuo hicho,Selemani Ubaya.
 Mkuu wa Chuo cha Ualimu cha Songea,Selemani Ubaya (kulia) akimuongoza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,Mh. Said Mwambungu kwenda kuzungumza na kugawa vyeti kwa wahitimu 502 chuoni hapo.
 Baadhi ya Wahitimu 502 wa Chuo cha Ualimu Songea katika ngazi ya stashahada,wakimsikiliza mkuu wa chuo hicho,Selemani Ubaya (hayupo picha) wakati wa mahafari ya 11 chuoni hapo.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,Mh. Said Mwambungu (kushoto) akisalimiana na Katibu wa Chama cha Walimu Mkoani humo,Bi. Luya Ngonyani alipowasili katika Chuo cha Ualimu cha Songea (matogoro) wakati wa mahafari chuoni hapo
Picha kwa hisani ya Michuzi Blog

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa