Home » » Barabara ya Songea, Tunduru-Mtwara kuanza kujengwa

Barabara ya Songea, Tunduru-Mtwara kuanza kujengwa

MKOA wa Ruvuma utakuwa na fursa nyingi za kiuchumi na maendeleo mara baada ya kufunguka kwamtandao wa barabara ndani yakipindi kifupi kijacho ambapo  kilometa 1,500  za kutoka Songea, Tunduru hadi Mtwara zitakuwa zimejengwa kwa kiwango cha lami kwa kipindi cha kuanza mwaka huu wafedha wa 2013/14.

Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muunganowa Tanzania, Mizengo Pinda wakati akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma,katika mkutano wahadhara wakati akiwa katika ziara ya siku nane ya kukagua shughuli za maendeleo za mkoa huo.

Pinda amesema kwasasa mkoa huo unamiradi mingi ya barabara ambayo ipo katika hatuaza mwisho za upembuzi wa kina na hivyo muda si mrefu ujezi wa barabara hizo utaanza.

Amesema barabaraya Songea hadi Namtumbo ambayo ni ya kilometa 73 kwa sasa ipo katika hatua ya mwisho kabisa ya umaliziaji baada ya kuweka lami na  ndani ya miezi michache itakabidhiwa kwa serikali.

Aidha Pinda amesema kwamba, Mkoa wa Ruvuma pia utaungani shwana Mkoawa Mtwara kwa ujenzi wa barabara ya Tunduru hadi Mangaka yakilometa 140, ambapo fedha zake zipo tayari ambazo zinato kaufadhili kutoka benki yamaendeleo ya Afrika na ujenzi wake utaanza mwezi ujao wa Agosti.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa