Home » » OCD MBINGA ALALAMIKIWA NA ASKARI

OCD MBINGA ALALAMIKIWA NA ASKARI

      
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEivD3fZqaty8yE_pL8Pvs2kK8PVIJ_ToW83JGmb4vzSmY6H61XqLI1Xdita4Lv-gMiNCBSgQbNi841xShX_SmPYCo7XCmwYnX9T3YKtQkLCzzOc_BS8jE35dWPYruGRPYTimHC_FD8HDpI/s1600/Police1.jpg

Na Muhidin Amri–Mbinga
BAADHI ya askari polisi wa kituo kikuu  Mbinga mjini,wamemtuhumu mkuu wa polisi wa wilaya hiyo(OCD)Jastine Joseph kuwa ni mtu anayetumia madaraka yake vibaya kwa kuendesha manyanyaso dhidi ya askari wa vyeo vya chini na kumuomba Mkuu wa jeshi ilo Said Mwema kumuondoa haraka kabla ya hali haijawa mbaya zaidi.
 
Wakizungumza na mtandao huu  kwa masharti ya kutotajwa majina yao,askari hao wamelalamika kuwa OCD wao amekuwa akitoa lugha za dharau na hata  zisizopendeza kwao hali inayowavunja moyo wa kazi askari wengine katika wilaya hiyo.
 
Walisema,iwapo jeshi litashindwa kumuhamisha Jastine kunaweza kutokea maafa makubwa kwani hawatoweza kuvumilia vitendo vinavyofanywa na afisa huyo hasa ukizingatia kuwa na wao ni watu wakubwa tena wenye familia kama yeye hivyo kitendo cha kuwatolea lugha za kiuni ni sawa na kuwadhalilisha.
 
Aidha wameshauri hata maafisa wengine katika wilaya hiyo wanatakiwa kuondoka kwani wameshaaka Mbinga kwa muda mrefu hivyo ni vema kupelekwa katika maeneo mengine ya nchi ili wakapate changamoto mpya za utendaji wa kazi, na kuendelea kuwepo katika wilaya hiyo ni tatizo kubwa kwani wameshafahamika na watu wengine hali inayowafanya kushindwa kuchukua maamuzi sahihi.
 
Wamesema ocd wao ni mtu hasiyetaka ushauri kutoka kwa mwingine hata kwa maafisa wenzake jambo linalomfanya kutengwa na kujikuta na yuko pekee yake au na wale askari wa kabila lake tu jambo lililowafanya askari kuwepo katika makundi hasa baada ya kufika Jastine kitu ambacho siku za nyuma hakikuwepo na askari wote walikuwa ndugu moja wakiishi na kusaidiana tofauti na sasa.

“huyu mkuu wetu ni tatizo kubwa,sijui hata mtu aliyempendekeza kuwa OCD ametumia kigezo gani,hafai kabisa yeye  kazi yake ni majungu tu na sio vinginevyo”alisema mmoja wa askari hao.
 
Kwa upande wake Jastine alikanusha tuhuma hizo na kuziita kuwa ni unafiki unaofanywa na askari wachache waliozoea kula rushwa kila mara hasa kwa waendesha pikipiki jambo ambalo yeye hataki kusikia katika uongozi wake.
“hizo tuhuma sio za kweli,zinafanywa na baadhi ya askari wngu hasa wale wala rushwa,nimeshaelekeza wakikamata pikipiki waje na faini hapa au mmiliki wake sio kuleta pikipiki hatuna eneo la kupaki kwani hizi tulizonazo ni nyingi na hatuna sehemu ya kuzipeleka”alisema.
 
Naye Kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki alikiri kuwepo kwa malalamiko  ya askari wa vyeo vya chini dhidi ya OCDwao na kuhaidia kuwa atashughulikia tuhuma hizo ili kupata ukweli wa jambo ilo.
“sisi hatufanyi mambo kwa kukurupuka tu lazima tufanye uchunguzi  ili tujiridhishe,unajua ukishakuwa kiongozi unatakiwa kuwa makini  hasa  katika maamuzi ili usifanye mambo kwa kumuonea mtu lazima utende haki kila wakati”alisema RPC

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa