Home » » BRELA YAWAFUNDA WAFANYABIASHARA SONGEA

BRELA YAWAFUNDA WAFANYABIASHARA SONGEA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Brela yawafunda wafanyabiashara Songea
WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (Brela) imeendelea kuwasisitiza wafanyabiashara kujitokeza kusajili majina ya biashara zao, ili ziweze kurasimishwa.
Akizungumza kwenye semina ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara mjini hapa juu ya umuhimu wa kusajili majina ya biashara zao, Msajili Msaidizi wa Brela, Seka Kasera, alisema wakisarasimisha biasha zao kunaisaidia serikali kuwatambua katika mikoa husika.
“Ni muhimu kwa wafanyabiashara kusajili, ili kutoa wigo mpana kwa serikali kuweka mipango yake ikiwa ni pamoja na suala nzima la ukusanyaji wa kodi,” alisema Kasera.
Alisisitiza kuwa kwa kufanya hivyo kutasaidia wafanyabiashara hao kuweza kupata mikopo kwa urahisi katika taasisi mbalimbali za kibenki ambazo zimekuwa hazina imani kwa kiasi kikubwa na watu ambao hawajasajili biashara zao.
Kasera alisema mafunzo ambayo Brela imekuwa ikiyatoa kwa wafanyabiashara yamewasidia kuwajengea uwezo na kutambua umuhimu wa kusajili majina ya biashara.
chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa