Home » » WATUHUMIWA WIZI WA PIKIPIKI WAUAWA

WATUHUMIWA WIZI WA PIKIPIKI WAUAWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

WATU wawili wanaodhaniwa kuwa majambazi wameuwawa na wananchi wenye hasira baada ya kutaka kupora pikipiki mbili walizokuwa nao madereva wa bodaboda, mtaa wa Mahilo kata ya Matogoro Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msikhela alithibitisha kutokea kwa mauaji ya watu hao juzi saa 3 usiku na kusema majina ya marehemu hao hayakufahamika mara moja.
Kamanda Msikhela alisema siku ya tukio Furko Alfonsi (24) dereva wa pikipiki yenye namba za usajili T.558 CJJ na Vasco Dagama (21) ambaye ni fundi na dereva wa pikipiki yenye namba za usajili T.363 BPL walioporwa pikipiki hizo kwa muda tofauti.
Alisema waliporwa pikipiki hizo baada ya kuwekewa kizuizi cha kamba ya manila iliyofungwa kwenye miti miwili mikubwa pembezoni mwa barabara.
Kamanda huyo alidai kwamba waporaji wanakadiriwa kuwa watano, walikuwa na silaha za jadi ambazo ni mapanga, nondo na kamaba za Manila ambao walijipanga kando ya barabara wakiwa na matawi ya miti yalitumika kuwapiga usoni waendesha pikipiki hao.
Alisema baada ya majambazi hayo kugundua kuwa Furko amepoteza fahamu na baadae walidhani amekufa walimbeba na kumtupa korongoni kisha waliendelea na uporaji wao ambapo walimzuia Vasco ambaye naye alishushiwa kipigo na kutoroka wakiwa na pikipiki hizo.
Kwa mujibu wa kamanda huyo Furko alipata fahamu baadaye na kujivuta hadi kwenye makazi ya watu na kuwajulisha yaliyojiri ndipo wananchi hao walipojikusanya kwa lengo la kuwasaka watuhumiwa hao kwa kuweka kizuizi kwenye barabara ya kutoka Mahilo kwenda  Songea mjini ghafla watuhumiwa wakiendesha pikipiki hizo huku wamemebana walisimamishwa na wanachi hao kabla ya kushushiwa kipigo ambapo watatu kati yao walitokomea kusikojulikana.
Alisema kuwa majambazi hao wawili walifariki dunia njiani wakati wanakimbizwa kwenda kwenye hospitali mkoa ya Songea na maiti zao zimehifadhiwa hapo huku wananchi wakitakiwa kwenda kuzitambua.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa