Home » » LAPF YATAKA UHURU KWA WATUMISHI

LAPF YATAKA UHURU KWA WATUMISHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
LAPF yataka uhuru kwa watumishi
MFUKO wa Pensheni kwa Watumishi wa Serikali za Mitaa (LAPF), umewataka waajiri kuacha tabia ya kuwalazimisha watumishi wao kujiunga na mifuko mingine badala yake watekeleza sheria namba 8 ya mwaka 2008, kifungu namba 30 kinachotoa uhuru kwa waajiriwa kuchagua mfuko wanaoutaka.
Wito huo ulitolewa na Meneja wa LAPF kanda ya Kaskazini, Rajabu Kinande wakati akitoa mafunzo kwa watumishi wa idara mbalimbali wa halmashauri hiyo ambao ni wanachama wa mfuko huo.
Alisema kuwa waajiri watende haki kwa kuwaacha wananchama waamue sehemu ya kwenda kujiunga kwani mifuko ya kijamii sio maadui, hivyo kila mtumishi anayo haki ya kuchagua mfuko anaotaka kujiunga nao.
Kinande alifafanua kuwa, lengo la mafunzo hayo kwa wananchama wake ni kutoa elimu kwani wamegundua kuwa kuna baadhi ya wanachama hawafahamu vizuri juu ya mfuko huo.
Kwamba, wanataka pia kujua wanachama wao wana maoni gani pamoja na kero zao ili waweze kuzifanyia kazi na kuboresha huduma za LAPF kwa lengo la kuleta tija.
Baadhi ya wanachama wa mfuko huo, walipongeza hatua hiyo ya kupatiwa elimu mara kwa mara tofauti na mifuko mingine ya kijamii, kwamba hawana mashaka kutokana na elimu wanayoipata juu ya mikopo na mafao yao.
Chanzo:Tanzania daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa