Home » » DKT. NDUMBARO AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUZINGATIA UADILIFU, KUJITUMA NA KUWAJIBIKA KWA WANANCHI

DKT. NDUMBARO AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUZINGATIA UADILIFU, KUJITUMA NA KUWAJIBIKA KWA WANANCHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro akitoa maelekezo mbalimbali ya masuala ya kiutumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi ya kuhimiza uwajibikaji mkoani Ruvuma. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hamashauri ya Wilaya ya Madaba Bw. Shafi Mpenda na kushoto kwakwe ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Bw. Bwai Biseko.
Baadhi ya watumishi wa Hamashauri ya Wilaya ya Madaba wakisikiliza kwa makini maelekezo ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro (hayupo pichani) aliyoyatoa katika halmashauri hiyo, wakati ziara yake ya kikazi ya kuhimiza uwajibikaji mkoani Ruvuma.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma, Bw. Biseko Bwai akitoa taarifa ya utekelezaji wa masuala ya kiutumishi kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro katika siku ya kwanza ya ziara ya kikazi ya Katibu Mkuu huyo mkoani Ruvuma yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijiji Bw. Simon Bulenganija akitoa taarifa ya utekelezaji wa masuala ya kiutumishi Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro katika siku ya kwanza ya ziara ya kikazi ya Katibu Mkuu huyo mkoani Ruvuma, yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.
Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Ibrahim Mahumi akitoa maelekezo kwa watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijijini kuhusu taratibu zinazohusu menejimenti ya Rasilimaliwatu serikalini, wakati wa ziara ya kikazi ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro ya kuhimiza uwajibikaji.
Baadhi ya watumishi wa Hamashauri ya Wilay ya Songea Vijiji wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro (hayupo pichani) katika siku ya kwanza ya ziara ya kikazi ya katibu mkuu huyo ya kuhimiza uwajibikaji katika Hamashauri hiyo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro amewataka Watumishi wa Umma nchini kuzingatia uadilifu katika utendaji kazi, kujituma, kuwajibika kwa wananchi na kwa Serikali ili kujenga Utumishi wa Umma uliotukuka.

Dkt. Ndumbaro amesema hayo, katika ziara yake ya kikazi ya siku tano mkoani Ruvuma yenye lengo mahususi la kubaini changamoto zinazowakabili Watumishi wa Umma katika maeneo yao ya kazi na kuzitafutia ufumbuzi ili kuwawezesha watumishi kutekeleza majukumu yao ipasavyo, ikiwa ni pamoja na kuwasisitiza Watumishi wa Umma juu ya mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Dkt. Ndumbaro akiwa katika Halmashauri za Wilaya ya Madaba na Songea Vijijini amewaeleza watumishi wa halmashauri hizo kuwa, misingi ya uadilifu na uwajibikaji itajengwa na watumishi hao kwa kubadili utamaduni wa kufanya kazi kwa mazoea (business as usual).

Dkt. Ndumbaro amesema kwamba, Wakurugenzi pamoja na Wakuu wa Idara nchini wana jukumu kubwa la kusimamia utendaji kazi katika maeneo yao ya kazi ili kubadilisha tabia za baadhi ya watumishi wasiowajibika ipasavyo, na kuwafanya watekeleze wajibu wao kwa bidii na kwa uadilifu mkubwa.

“ Ninyi Wakurugenzi na Wakuu wa Idara mhakikishe mnahimiza nidhamu kwa Watumishi wa Umma katika maeneo yenu, mtumishi akikosea achukuliwe hatua mara moja kwa mujibu wa Sheria , Kanuni na Taratibu za Utumishi wa umma zilizopo” Dkt. Ndumbaro amefafanua.

Dkt. Ndumbaro amebainisha kuwa, kama kuna watumishi wasiotimiza wajibu wao na hawachukuliwi hatua zozote za kinidhamu au za kisheria dhidi yao, kitendo hicho huwakatisha tamaa watumishi wanaojituma katika utendaji kazi wao.

Aidha, Dkt. Ndumbaro amekemea tabia iliyojengeka kwa baadhi ya watumishi ya kuwakatisha tamaa watumishi wanaojituma na wanaozingatia maadili. “Viongozi tusipokemea na kuwachulia hatua watumishi wenye tabia ya kuwabeza na kuwakatisha tamaa watumishi wanaojituma kazini, ni dhahiri kuwa itashusha morali ya utendaji kazi wa watumishi wanaochapakazi” Dkt. Ndumbaro amesisitiza.

Dkt. Ndumbaro amewataka Wakurugenzi na Wakuu wa Idara kuwatambua watumishi wanaofanya kazi kwa bidii kwa kuwapa moyo na motisha, ikiwa ni pamoja na kuwaandikia barua za kuwapongeza ama kuwapa vyeti ikiwa ni mkakati wa kukuza utamaduni wa watumishi kupenda kufanya kazi.

Pia, Dkt. Ndumbaro hakusita kuwasisitiza Maafisa Utumishi, Watumishi wa Masijala na Makatibu Mahususi kuwa na lugha nzuri wakati wa kuwahudumia wateja wa ndani na wa nje pindi wanapofika kwao kupata huduma.

Dkt. Ndumbaro anaendelea na ziara ya kikazi ya kuhimiza uwajibikaji mkoani Ruvuma katika Halmashauri za Wilaya ya Songea Mjini, Tunduru, Mbinga, Nyasa, na Namtumbo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa