Home » » WAZIRI MKUU AAGIZA WANAKIJIJI 21 KUFIDIWA ARDHI KABLA YA KRISMASI

WAZIRI MKUU AAGIZA WANAKIJIJI 21 KUFIDIWA ARDHI KABLA YA KRISMASI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Imeandikwa na Mwandishi Wetu
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Chomolo wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma, wakati waliposimamisha msafara wake jana ili kuzungumza naye. Waziri Mkuu alikuwa anaelekea Tunduru kuendelea na ziara ya kikazi mkoani humo. (Picha na Ofi si ya Waziri Mkuu).
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amempa mwezi mmoja Ofi sa Ardhi wa wilaya ya Namtumbo, mkoani Ruvuma, Maurus Yera awe ametafuta ardhi ya kuwafi dia wakazi 21 wa kijiji cha Lwinga wilayani humo ambao eneo lao lenye ukubwa wa ekari 101 lilitwaliwa na serikali mwaka 2008.
Eneo hilo lilitwaliwa kupisha ujenzi wa shule ya sekondari ya mkoa wa Ruvuma. Alitoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi hao kupitia mabango, ambapo walimuomba awatatulie kero hiyo ya madai ya fidia ya ardhi iliyodumu kwa miaka 10 bila kupatiwa ufumbuzi.
Waziri Mkuu alisema haoni sababu ya Halmashauri hiyo kushindwa kuwafidia wananchi hao sehemu ya ardhi kwa muda wote huo ukizingatia wilaya hiyo ina hifadhi ya ardhi.
“Nataka wananchi hawa wawe wamelipwa fidia yao ya ardhi kabla ya siku kuu ya Krismasi ya mwaka huu. Serikali haiko tayari kuona wananchi wake waliotoa ardhi kupisha maendeleo wakisumbuliwa,” alisema.
CHANZO HABARI LEO 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa