Home » » Kampuni 12 zaruhusiwa kununua korosho

Kampuni 12 zaruhusiwa kununua korosho

KAMATI ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma imezipitisha kampuni 12 kuchuana katika ununuzi wa korosho za wakulima zikiwa ni juhudi za Serikali kuwaondolea kero hiyo.
Pamoja na maamuzi hayo, pia Kamati hiyo imetakiwa kuwalipa wakulima Sh 1,100 au zaidi kwa kilo moja na kwamba mfumo huo hautaruhusu utaratibu wa kuwakopa wakulima hao kuanzia Novemba 22 mwaka huu.
Akitangaza maamuzi hayo, Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Chande Nalicho alisema maamuzi hayo yamefikiwa katika kikao kilichoketi Novemba 21 mwaka huu.
Nalicho amewatahadharisha walanguzi walionunua korosho hizo kutoka kwa wakulima kwa kupitia vipimo haramu vya kangomba kuwa hawatapewa mwanya wa kuuza wala kusafirishaa korosho hizo kutoka nje ya wilaya hiyo na kwamba atakayenaswa Sheria itafuata mkondo wake.
Katika taarifa hiyo, Nalicho alizitaja kampuni hizo kuwa ni Export Trading Co. Limited, Prayosa, Kulaathool Co. Ltd, Shareeji Impex Ltd, Saidi Mohamed Said pamoja na Kampuni Kongwe ya Olam Tanzania Ltd.
Nyingine ni China Pesticide Tanzania Ltd, Amina Seti, Saweya Impex Tanzania Ltd, Alpha Choice Ltd, Sunrise Commodities pamoja na Chama Kikuu cha Ushirika cha Wakulima wa korosho Wilayani Tunduru (TAMCU Ltd).
Chanzo;Habari Leo




0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa